logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nyako ameokoa maisha yangu aliyekuwa mtagazaji Kimani mbugua asema

Kimani ametaja pesa alizopata zimemuazishia upya maisha

image
na Davis Ojiambo

Burudani28 November 2023 - 11:31

Muhtasari


  • •Kimani alisimulia kua kwa sasa ana weza kujikimu maisha kwa kuwa na uwezo wa kulipia mahitaji yake
Kimani Mbugua na Nyako

Aliyekuwa mtangazaji, Kimani Mbugua ameeleza jinsi mwanatiktoker maarufu nchini Nyako amebadilisha maisha yake baada ya mchango wa zaidi ya nusu milioni  kupitia wafuasi wake wa mitandao.

"Nyako alibadilisha maisha yangu sikuwa  na mfahamu ila kwa sasa amekuwa mtu wa kupigiwa mfano kwa maisha yangu jinsi alivyojitokeza na kusikia kilio changu aliweza kuwashawishi wafuasi wake kunichangia pesa ambazo kwa sasa nafurahi kwa kuwa nimeanza maisha yangu upya,"alisema.

Kulingana na Kimani Mbugua mwanatiktoker huyo alikuwa  msamaria mwema ambaye alitumwa na muumba wake kumaliza kilio chake na kumuwezesha kupata fahamu ya maisha kwani kwa sasa amepata nyumba ya kukodi na anaweza kumudu mahitaji yake.

Kimani kwa sasa amesimulia kuwa maisha yake yamerudi hali ya kawaida huku akimshukuru Nyako kwa jinsi alijitokeza kuokoa maisha yake.

"Namshukuru sana Nyako kwa mchango wake na ushauri mwema jinsi ambavyo ningetumia pesa hizo kufanikisha ndoto ya maisha yangu tena,"alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved