logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Wamerudiana?” Picha ya Samidoh akifurahia muda na Edday Nderitu yazua msisimko mtandaoni

Staa huyo wa Mugithi alirejea nchini Kenya hivi majuzi lakini Bi Edday Nderitu na watoto wao watatu waliachwa Marekani.

image
na Radio Jambo

Habari14 February 2024 - 11:29

Muhtasari


•Picha Samidoh akiwa na Edday Nderitu imekuwa ikivuma kwenye mitandao mbalimbali na kuzua hisia mseto.

•Staa huyo wa Mugithi alirejea nchini Kenya hivi majuzi lakini Bi Edday Nderitu na watoto wao watatu waliachwa Marekani.

wakifurahia muda pamoja

Picha ya staa wa Mugithi, Samuel Muchoki almaarufu Samidoh akiwa na mzazi mwenzake Edday Nderitu imekuwa ikivuma kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kuzua hisia mseto kutoka kwa watumiaji wa mitandao.

Picha inayowaonyesha wanandoa hao wa zamani wakiwa katika hali ya furaha ilichapishwa kwa mara ya kwanza na meneja wa Samidoh, Moses Marite kabla ya watumiaji wengine wa mitandao ya kijamii kuisambaza

Mashabiki wa wawili hao wameendelea kueleza kuchanganyikiwa kwao mtandaoni, baadhi wakipendekeza kuwa wazazi wenza hao huenda wamerudiana huku wengine wakipendekeza kwamba huenda walikutana ili kuzungumza kuhusu watoto wao.

Picha hiyo huenda ilipigwa wakati wa ziara ya hivi majuzi ya Samidoh nchini Marekani ambako alienda kuwatembelea watoto wake baada ya miezi mingi ya kuwa mbali nao.

Staa huyo wa Mugithi alirejea nchini Kenya hivi majuzi lakini Bi Edday Nderitu na watoto wao watatu waliachwa Marekani ambako wamekuwa tangu mapema mwaka jana.

Bi Edday Nderitu kwa sasa anaishi nchini Marekani pamoja na watoto wao. Aliondoka nchini mapema mwaka jana na anaonekana tayari kutulia huko vizuri huku watoto wakiwa wameanza shule huko.

Mwezi Julai mwaka jana, Bi Edday Nderitu aliweka wazi kwamba alimuacha mumewe ili awe na mwanamke ambaye alionekana kumtaka zaidi.

"Wacha nifafanue mambo machache ambayo yalishirikiwa mtandaoni na sio sahihi. Siko kwenye ndoa ya wake wengi, kama ilivyoelezwa nilimuacha mume kwa yeyote aliyemhitaji zaidi,” Edday alisema kupitia Facebook.

Aliongeza, "Nilifanya uamuzi wa kujiondoa mimi na watoto wangu kutoka kwa mazingira hayo yenye sumu, haswa binti yangu kijana ambaye kwa bahati mbaya anapokea moja kwa moja tabia isiyoaminika iliyoonyeshwa."

Mara nyingi, Bi Edday Nderitu amesisitiza kwamba hayuko tayari kuwa kwenye ndoa ya wake wangi licha ya mpenzi wa Samidoh, seneta Karen Nyamu kusisitiza kwamba yuko tayari ku'share mume naye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved