logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mammito anawajibu wakosoaji kuhusu video ya Jowie

Klipu hiyo ambayo imesambaa kwa kasi imemshuhudia mcheshi huyo kupokea lawama kutoka kwa baadhi ya Wakenya ..

image
na Davis Ojiambo

Burudani14 March 2024 - 09:52

Muhtasari


  • Klipu huo ulijiri saa chache baada ya Jowie kuhukumiwa kifo katika mauaji ya Monica Kimani mnamo 2018.
mammito

Mcheshi Eunice Mammito  amevunja ukimya baada ya ukosoaji kuhusu video wa kimchezo alioutengeneza dhidi ya Jowie.

Mamito alitumia mtandao wake wa kijamii Alhamisi asubuhi akisema kuwa ni nadra kwa Wakenya kuungana na kumkemea.

Klipu huo ulijiri saa chache baada ya Jowie kuhukumiwa kifo katika mauaji ya Monica Kimani mnamo 2018.

Katika video hio , anadaiwa kumshauri Jowie kuona hukumu hiyo kwa manufaa yake binafsi.

Klipu hiyo ambayo imesambaa kwa kasi imemshuhudia mcheshi huyo kupokea lawama kutoka kwa baadhi ya Wakenya kwenye mitandao ya kijamii.

Akijibu, Mammito amesema kwa kejeli umoja wa kumkemea unampa matumaini kuwa siku moja Wakenya wataungana kuzungumza dhidi ya maovu mbalimbali yanayoikumba nchi, ikiwemo ufisadi.

"Nimeshuhudia tukio la nadra jambo ambalo halijatokea tangu mwaka 2002 watu kutoka kila hali wakiungana kunikemea."

"Inanipa matumaini kwa siku zijazo kwamba siku moja tutaungana na kupigana dhidi ya ufisadi na mambo mengine yanayoisumbua nchi yetu", Mammito alisema.

Jibu hilo pia limevutia dhihaka, huku wengine wakimshutumu Mammito kwa kutafuta huruma baada ya fujo alizoanzisha.

Wengi walimpigia debe kwa kutojali licha ya yaliyompata Jowie, na hata kukosa kuheshimu marehemu Monica Kimani kwenye skiti yake.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved