logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Ndoto yangu ni kuwa baba wa mabinti 3!” – Eric Omondi

“Kuhusu ndoa, sisi ni watu wa surprise. Lolote linaweza kutokea wakati wowote.”

image
na Radio Jambo

Habari08 May 2024 - 07:33

Muhtasari


• Kuhusu kufunga harusi kabisa na kumfanya Lynne kuwa mkewe rasmi, Omondi alisema;

 
• “Kuhusu ndoa, sisi ni watu wa surprise. Lolote linaweza kutokea wakati wowote.”

Eric Omondi

Mchekeshaji aliyegeuka na kuwa mwanaharakati Eric Omondi amezungumzia fahari ya kuwa baba kwa mtoto wa kike.

Akizungumza na blogu ya Rick Media baada ya kutua nchini Tanzania, Omondi alisema kuwa anajihisi angalau yuko katika mkondo salama kufanikisha ndoto yake.

Mwanaharakati huyo mwenye shughuli nyingi za kiharakati kando na familia alisema kuwa tangu utotoni, ndoto yake imekuwa kuitwa baba wa mabinti watatu, na kusema kwamba kumpata binti wa kwanza, Kyla ilikuwa kama mwanzo wa majibu kwa ndoto zake za utotoni.

“Mtoto wa kike ni wa baba, inakuja na hisia Fulani nzuri kwani Mungu alijibu maombi yangu. Mimi tangu utotoni nilikuwa nimeomba nipate watoto wa kike watatu. Nishampata mmoja, bado wawili,” Omondi alisema.

Omondi pia alizungumzia ukuaji wa bintiye Kyla na kusema kwamba ameshakua kwa kasi ya ajabu na ivyo itampa fursa yeye na mpenziwe Lynne kutathmini kupata watoto wengine wawili – mabinti – ili kutimiza ndoto yake ya utotoni.

“Kyla kashakua kwa haraka sana, yani unalala, unafumba na kufumbua, kakua,” alisema.

Kuhusu kufunga harusi kabisa na kumfanya Lynne kuwa mkewe rasmi, Omondi alisema;

“Kuhusu ndoa, sisi ni watu wa surprise. Lolote linaweza kutokea wakati wowote.”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved