logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamuziki Prezzo,aanguka akitumbuiza wageni

mwanamuziki maarufu wa Kenya Prezzo alianguka Hotelini Westwood katika uzinduzi wa The Bahati Empire

image
na Davis Ojiambo

Burudani07 June 2024 - 12:20

Muhtasari


  • •Furaha ya hafla hiyo ilichukua mkondo wa ghafla wakati Prezzo alipoanguka chini, akionekana kupata kifafa
  • •Tukio hili liliweka kivuli juu ya kile kilichokusudiwa kuwa hafla ya kusherehekea, na kusababisha wasiwasi 
Prezzo akubali yeye ni mtoto wa mama

Wakati wa makala ya The Bahati’s Empire, kipindi cha uhalisia cha televisheni kitakacho peperushwa kwenye Netflix Ijumaa, mwanamuziki maarufu wa Kenya Jackson Ngechu Makini almaarufu Prezzo alianguka akituumbuiza mashabiki.

Tukio hilo lililotokea Mei 6, lilivuta umati wa watu mashuhuri na wanahabari, huku Naibu Rais Rigathi Gachagua akihudhuria.

Furaha ya hafla hiyo ilichukuwa mkondo wa ghafla wakati Prezzo alipoanguka chini huku kiini cha kuanguka kwake kisijulikane kama inavyoonekana kwenye video zinazosambazwa mtandaoni.

Usaidizi wa haraka ulitolewa na waliohudhuria huku wakingojea usaidizi zaidi wa kimatibabu, ingawa mjadala fulani uliibuka kuhusu kufaa kwa msaada huo.

Tukio hili liliweka kivuli juu ya kile kilichokusudiwa kuwa hafla ya kusherehekea, na kusababisha wasiwasi na patashika kwa ustawi wa rapper huyo.

Wakati huo huo, uzinduzi wa The Bahati’s Empire, hatua muhimu kwa mwanamuziki Bahati na familia yake, uliendelea kama ilivyopangwa.

Bahati alielezea shukrani zake za dhati kwa mafanikio ya kipindi hicho, akihusisha na usaidizi usioyumba wa marafiki, familia, vyombo vya habari, na wafanyakazi wenzake wa tasnia, hasa kutambua jukumu la mke wake Diana Marua kama mtayarishaji mkuu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved