logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Nimekuwa na stress siku nzima nikifikiria pazia Khaligraph atatumia kwa jumba lake” – Dj Shiti

“Na imagine khaligraph atashonesha Curtains kiasi ganiii 🤔🤔 hiyo kitu imeni Stress the whole day,” Shiti aliandika katika picha yake akiwa ameshika kidevu akiwa amekalia kiti kidogo.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani13 November 2024 - 12:06

Muhtasari


  • Na imagine khaligraph atashonesha Curtains kiasi ganiii 🤔🤔 hiyo kitu imeni Stress the whole day,” Shiti aliandika katika picha yake akiwa ameshika kidevu akiwa amekalia kiti kidogo.
  • "Unaamka unapata unatrend sababu umejenga nyumba kubwa inakaa kama maduka, Mungu anajua haya ndio matatizo niliyokuwa natamani," Khaligraph alisema.



Mchekeshaji na muigizaji Dj Shiti ameibuka na utani kuhusu  kitu ambacho kimekuwa kikimnyima usingizi tangu wiki hii ilipoanza.

Kupitia Instagram, Shiti alikiri kwamba amekuwa akifikiria siku nzima hadi kupata msongo wa mawazo akijaribu kufikiria kuhusu pazia atakazotumia msanii Khaligraph Jones katika jumba lake kubwa.

Shiti alisema kwamba kila wakati anapojaribu kuketi chini na kutulia, anajipata akitafakari kiwango cha pazia ambazo rapa huyo wa ‘Mazishi’ atakuwa akishonewa ili kutoshea katika madirisha ya jumba lake la kipekee.

Na imagine khaligraph atashonesha Curtains kiasi ganiii 🤔🤔 hiyo kitu imeni Stress the whole day,” Shiti aliandika katika picha yake akiwa ameshika kidevu akiwa amekalia kiti kidogo.

Msanii Khaligraph Jones amekuwa gumzo la mitandao ya kijamii kwa takribani siku 3 sasa baada ya kuonyesha picha na video za jumba lake kubwa ambalo limezua mjadala mitandaoni.

Baadhi ya watumizi wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakitania jumba hilo wakilifananisha na jumba la biashara za jumla, huku wengine wakilifananisha na jumba la masomo ya chuo kikuu.

Hata hivyo, Jones alijitokeza akisema kwamba maoni ya watu kuhusu jumba lake hayamnyimi usingizi hata kidogo, akiweka wazi kwamba shida kama hizo ndizo alikuwa akiomba zimfuate kwa muda mwingi.

"Unaamka unapata unatrend sababu umejenga nyumba kubwa inakaa kama maduka, Mungu anajua haya ndio matatizo niliyokuwa natamani," Khaligraph alisema.

Awali, alidokeza kwamba muundo wa jumba lake huenda umechochewa na maisha ya kisanii ya rapa wa Marekani, Rick Ross ambaye pia anamiliki jumba la kipekee nchini Marekani.

Jones alisema kwamba kwa wale ambao hawajafika kwake, wajue kwamba madhari yenyewe ni kama mtu kuingia Marekani kwa jumba la Rick Ross.

Alionekana kutupa kijembe kwa wakosoaji wa jumba lake akisema watu wengi hawajazoea majumba ya muundo huo na ndio wanaobwabwaja kwenye mitandao ya kijamii.

“Hamjazoea hizi settings, hapa ukikuja ni kama umeingia Amerika, kwa Rick Ross. Heshima ni lazima kwa OG,” Khaligraph Jones alisema huku akicheka.

Siku ya Jumatatu, Jones alishangazwa na watu ambao walikuwa wanachapisha picha na video za jumba lake mitandaoni wakiambatanisha na kauli za dharau kuhusu mjengo huo.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved