logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Robert Burale asimulia kunyimwa nafasi ya kuhubiri kanisani kwa kupinga itikadi za LGBTQ

“Kuna baadhi ya wanaume kutoka taifa fulani la Afrika Mashariki na jamii Fulani hapa. Wanachukua wavulana wadogo na kuwalipa Ksh1,000 kwa shoti na wanawaharibu."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani14 November 2024 - 14:20

Muhtasari


  • Burale alisema kwamba msukumo wake kuhubiri dhidi ya LGBTQ ni kutokana na idadi kubwa ya vijana Nairobi anaowajua wanatembea na nepi kwa kulawitiwa.
  • “Kuna baadhi ya wanaume kutoka taifa fulani la Afrika Mashariki na jamii Fulani hapa. Wanachukua wavulana wadogo na kuwalipa Ksh1,000 kwa shoti na wanawaharibu. Vijana sasa wanatembea na nepi." 



Mchungaji Robert Burale amefichua kwamba aliwahi nyimwa nafasi ya kuhubiria vijana katika mkutano Fulani wa injili kutokana na misimamo yake mikali dhidi ya jumuiya ya mapenzi ya jinsia moja, LGBTQ.

Akizungumza na Dr Ofweneke kwenye podikasti ya Lessons @30, Burale alisema kwamba misimamo yake mikali dhidi ya LGBTQ ilimkosesha fursa ya kuhubiri baada ya viongozi wa mkutano huo wa injili kumtaka asizungumzie masuala ya LGBTQ katika mahubiri yake.

Hata hivyo, Burale alisema kwamba alikataa kusikilisha maelekezo yao na kufunga Biblia yake na kuondoka bila kuhubiria vijana kwenye mkutano huo.

“Aina yangu ya injili haikubiliwi katika baadhi ya mimbari. Nimewahi kataliwa nisihubiri kwa sababu nimetalikiwa, na pia nimewahi ambiwa kwamba ‘tunajua unazungumza sana dhidi ya LGBTQ, tafadhali kwenye mimbari hii legeza Kamba, hatuzungumzii masuala hayo hapa’. Niliwaambia mnajua nini, Mungu awabariki. Nikafunga Biblia yangu na kuondoka,” Burale alisimulia.

Hata hivyo, mchungaji huyo alifafanua kwa kiduchu kwamba tukio hilo halikumtokea nchini Kenya lakini ni katika nchi nyingine ambayo aliahidi siku moja atakuja kuiweka wazi na kuzungumzia hali nzima jinsi ilivyotokea.

Burale alisema kwamba msukumo wake kuhubiri dhidi ya LGBTQ ni kutokana na idadi kubwa ya vijana Nairobi anaowajua wanatembea na nepi kwa kulawitiwa.

“Kuna baadhi ya wanaume kutoka taifa fulani la Afrika Mashariki na jamii Fulani hapa. Wanachukua wavulana wadogo na kuwalipa Ksh1,000 kwa shoti na wanawaharibu. Vijana sasa wanatembea na nepi. Vijana wengi sasa hivi wanatembea wakiwa wamejifunga nepi na mtu Fulani anakuja kusema eti tusikemee suala hilo. Unajua utasema tusikemee hadi pale litakapofika mlangoni pako,” Burale alisema.

Awali, Burale alisema kwamba amewahi nyanyapaliwa mitandaoni kuwa ni iluminati kutokana na mapenzi yake kwa mavazi meusi.

“Wenye chuki hawawezi kusema chochote cha hakika, kuna mtu aliniita pasta wa iluminati eti ndio maana nahubiri nikiwa nimevaa nguo nyeusi. Ukweli ni kwamba mimi napenda nguo nyeusi na nitaendelea kuvaa nguo nyeusi. Mimi navaa suti nyeusi na hata boxer nyeusi, ni vile tu siwezi onyesha,” Burale alisema.

Burale alisema kwamba matukio kama hayo yamemfanya kubana idadi ya marafiki zake, akisema kuwa yeye ana marafiki 4 tu.


 


 


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved