logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Imefika stage ya kuongea kizungu sasa!” – Mulamwah aonyesha maendeleo ya jumba lake kijijini

“Proud of Khaligraph Jones, kitu umefanya ain’t easy to achieve. to anyone else out there its all possible - baraka tele , Mungu mbele,” aliongeza Mulamwah.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani16 November 2024 - 09:40

Muhtasari


  • “Proud of Khaligraph Jones, kitu umefanya ain’t easy to achieve. to anyone else out there its all possible - baraka tele , Mungu mbele,” aliongeza Mulamwah.
  • Mulamwah amekuwa akishughulika juu chini kukamilisha ujenzi wa jumba lake la kifahari kijijini Kitale kwa zaidi ya miaka miwili sasa.



Mchekeshaji Kendrick Mulamwah ameonyesha maendeleo ya ujenzi wa jumba lake la kifahari kijijini.

Mulamwah alifurahi akifichua kwamba ujenzi hupo unakaribia kukamilika, huku akisimulia jinsi ni gharama ghali kumalizia ujenzi kuliko kuanza.

Mchekeshaji huyo alitania akisema kwamba jumba lake sasa limefika hatua ya kuzungumza Kizungu, akimaanisha kwamba limenaza kuleta muonekano wake halisi kama ilivyokuwa kwenye mchoro.

Maskani inakuja pole pole tu, kumaliza ndio joto lakini almost done 💪, nyumba inaongea kizugu sasa 😂. pace ni pole pole tu let no one pressure you.move slow move correctly,” Mulamwah alisema.

Mtangazaji huyo wa redio pia alichukua nafasi hiyo kumhongera rapa Khaligraph Jones kwa ujenzi wa jumba la kipekee viungani mwa mji wa Ngong.

Kwa mujibu wa Mulamwah, ambacho amekifanya Khaligraph Jones si cha kuchukuliwa kwa mzaha kwani kujenga jumba mpaka kulikamilisha si kazi rahisi.

“Proud of Khaligraph Jones, kitu umefanya ain’t easy to achieve. to anyone else out there its all possible - baraka tele , Mungu mbele,” aliongeza Mulamwah.

Mulamwah amekuwa akishughulika juu chini kukamilisha ujenzi wa jumba lake la kifahari kijijini Kitale kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Mchekeshaji huyo alianza ujenzi wa jumba hilo mapema 2022 baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Carrol Sonie.

Hata hivyo, kwake amekuwa akipata faraja kwa methali ya pole pole ndio mwendo, akiendeleza ujenzi wake.

Kwa upande mwingine, Khaligraph Jones amekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii kwa wiki sasa baada ya kuonyesha mjengo wake uliokamilika.

Muundo na muonekano waq mjengo huo ulizua gumzo mitandaoni, baadhi wakiutania kuwa ni mkubwa kupita kiasi na kwamba halifahi kuwa jumba la makazi ya kibinafsi bali jumba la biashara ama taasisi ya masomo.

Khaligraph alionekana kutoyumbishwa na kauli hizo za husda, akisema kwamba ndoto yake ni kuishi maisha kama rapa wa Marekani, Rick Ross.

Jones alisema kuwa anapoona watu wanamzungumzia katika mitandao ya kijamii kisa jumba lake kubwa, shida kama hizo ndizo alikuwa akiota kumtokea miaka mingi iliyopita.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved