logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa msanii wa sekula, Kush Tracey abatizwa, miaka 4 baada ya kuokoka

Alifafanua kwamba miaka 4 iliyopita, alipokea ubatizo wa roho mtakatifu lakini sasa ,amepokea ubatizo wa maji kusimika kabisa uhusiano wake na Mungu.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani25 November 2024 - 14:00

Muhtasari


  • Alifafanua kwamba miaka 4 iliyopita, alipokea ubatizo wa roho mtakatifu lakini sasa ,amepokea ubatizo wa maji kusimika kabisa uhusiano wake na Mungu.
  • Alichukua nafasi hiyo kuelezea uelewa wake kuhusu umuhimu wa ubatizo kwa Wakristo.




ALIYEKUWA msanii wa miziki ya kidunia, Kush Tracey hatimaye amempokea roho mtakatifu kupitia ubatizo, miaka minne baada ya kuanza safari yake ya wokovu.

Kush Tracey kupitia ukurasa wake wa Instagram, alichapisha video akifanyiwa ubatizo kwenye dimbwi la maji ambapo alisema kwamba imekuwa ni safari ya miaka 4 ambayo hawezi kuijutia hata kidogo.

Alifafanua kwamba miaka 4 iliyopita, alipokea ubatizo wa roho mtakatifu lakini sasa ,amepokea ubatizo wa maji kusimika kabisa uhusiano wake na Mungu.

“Imekuwa miaka 4 ya kutembea na Bwana & Mwokozi wangu Yesu Kristo🥳 na tangu nilipopokea Ubatizo wa Roho Mtakatifu (wakati Roho Mtakatifu anaingia katika maisha ya waumini na kuwatia nguvu kwa ajili ya huduma ya Mungu) na leo hatimaye nimebatizwa katika maji,” Tracey alitangaza kwa furaha.

Alichukua nafasi hiyo kuelezea uelewa wake kuhusu umuhimu wa ubatizo kwa Wakristo.

“Ubatizo maana yake halisi ni kuzamishwa kabisa na ni ishara ya nje ya mabadiliko ya ndani ambapo mtu hujitangaza hadharani kuwa ni wake na kujitambulisha na Yesu Kristo kwa kawaida hufanyika baada ya mtu kuwa mwamini mpya ambaye amezaliwa mara ya pili.”

Hata hivyo, kwa kutumia vifungu vya Biblia, Tracey alifafanua kwamba ubatizo katika maji si njia ya pekee ya mtu kujenga uhusiano wake na Mungu kupitia kuamini katika uwepo wa maisha baada ya kifo.

Alisema kwamba wakristo hata baada ya ubatizo, wana jukumu la kutumikia wokovu wao kwa woga mkuu mbele pa Mungu, akitoa kifungu hicho kwenye kitabu cha Wafilipi 2:12.

Mnamo mwaka 2021 wakati alifunguka kwa mara ya kwanza kuhusu uamuzi wake wa kutafuta maisha mapya katika Ukristo, Tracey alifichua kwamba maisha yake yalikuwa yamechukua mkondo mbaya usioweza kuelezeka.

Alipoulizwa kwa nini aliokolewa, Kush alisema;

"Nilikuwa nimegonga mwamba sana, watu wangeniona kwenye TV na kwenye mitandao ya kijamii lakini nyuma ya hapo nilikuwa nikipambana na hisia tofauti.”

“Nilihisi kuna maisha zaidi na kuwepo kwangu mbali na kuachilia muziki na kujulikana. Nikifa leo watu wangesema nini kunihusu?”

“Nilihitaji kupata zaidi na kuishi katika kusudi na ningeweza tu kupata hiyo katika Kristo. Kuwa Mkristo ni ngumu sana, unapaswa kuwa na nia na kila mtu. Huwezi kutenda jinsi unavyotaka, kuwa Mkristo ni dhabihu kubwa ambayo ni ngumu kufanya maishani mwangu."

Kuhusu kama alijisikia kukaribishwa na Wakristo wengine katika tasnia ya burudani, Kush Tracey alishiriki;

“Kwangu mimi wokovu haukuwa wa watu kunikubali, watu wanafanya mambo kwa sababu wana ajenda tofauti. Kuna watu wapo hapa kwa ajili ya biashara, wengine ni waaminifu kwa Mungu. Ninaamini katika kufuata kile ambacho Mungu ameniitia kufanya.”

“Mungu amekuwa akiniunganisha na mambo, Wakati kitu kinatoka kwa Mungu huna haja ya kukipigania."


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved