logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shakib Cham Atoa Onyo Kali Kwa Wanaoeneza Uvumi Kwamba Anam’cheat Mkewe, Zari

"Nataka kuweka mambo wazi, baadhi ya wanawake ni wateja wa thamani na wafuasi wa ukusanyaji wa King Cham. Hawajihusishi nami kimahaba, wala sina nia yoyote ya kujihusisha nao."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani02 December 2024 - 10:19

Muhtasari


  • Zari na Shakib wameoana kwa mwaka mmoja, baada ya kufunga ndoa ya Kiislamu – nikkah – iliyofanyika faraghani mwaka jana.
  • Baadae mwezi Oktoba, waliweka mambo wazi kwa kuandaa sherehe kubwa ya harusi nchini Afrika kusini.
  • Harusi hiyo ya kifahari ilihudhuriwa na watu mashuhuri na baadhi ya wasanii wa Young Famous na Afrika.



MFANYIBIASHARA Shakib Cham Lutaaya ametoa onyo kali kwa baadhi ya wanablogu wanaoeneza taarifa alizozitaja kama uvumi kwamba anachepuka katika ndoa yake.

Kupitia kwa aya ndefu alizochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram kupitia insta-story, Shakib alisema kwamba amekuwa akifumbia macho tetesi hizo kwa muda lakini sasa anaona kimya chake kinachukuliwa kama unyonge.

Shakib alisema kwamba hajui mtu aliyebuni na kuibuka na uvumi kwamba ana mpenzi mwingine nje ya ndoa yake na Zari, na kukanusha taarifa hizo akizitaja kuwa za kupotosha.



"Wapendwa wa mitandao ya kijamii na mashabiki, ningependa kushughulikia suala linalonihusu kuhusu uvumi wa hivi majuzi wa magazeti ya udaku kwamba nina uhusiano wa kimapenzi nje ya ndoa yangu. Imefika akilini mwangu kuwa kumekuwa na hadithi za uwongo zinazosambaa zikionyesha kuwa ninamsaliti mke wangu,” Shakib alisema.

Akizungumzia kuhusu baadhi ya wanawake anaoonekana nao na ambao sekeseke zilikuwa zinadai kuwa ni wapenzi wake, Shakib alisema kwamba wao ni wateja wake katika duka lake la nguo.

"Nataka kuweka mambo wazi, baadhi ya wanawake ni wateja wa thamani na wafuasi wa ukusanyaji wa King Cham. Hawajihusishi nami kimahaba, wala sina nia yoyote ya kujihusisha na mahusiano ya faragha nao au wanawake wengine wowote kwa jambo hilo. Kama mwanamume aliyeoa, mapenzi yangu na kujitolea viko kwa mke wangu,” alisisitiza.

Zaidi ya hayo, Shakib aliwasihi mashabiki na wafuasi wake kupuuza madai hayo akiyaita uvumi na propaganda zisizo na msingi ambazo zingedhuru ndoa yake.

"Ninaomba kila mtu tafadhali ajiepushe kueneza uvumi na propaganda hizi zisizo na msingi, kwani sio tu sio za kweli lakini pia zinadhuru kwa ndoa yangu, sifa ya kibinafsi na kitaaluma. Hebu sote tuonyeshe kuelewana na kuheshimiana.”



Zari na Shakib wameoana kwa mwaka mmoja, baada ya kufunga ndoa ya Kiislamu – nikkah – iliyofanyika faraghani mwaka jana.

Baadae mwezi Oktoba, waliweka mambo wazi kwa kuandaa sherehe kubwa ya harusi nchini Afrika kusini.

Harusi hiyo ya kifahari ilihudhuriwa na watu mashuhuri na baadhi ya wasanii wa Young Famous na Afrika.

Hata hivyo, unaambiwa sio vyote ving’aavyo ni dhahabu. Ndoa ya wawili hao imekumbwa na misukosuko si haba katika kipindi hicho, suala luu la ugomvi likiwa ni ukaribu wa Zari na babydaddy wake, Diamond Platnumz.

Miezi michache iliyopita, Shakib na Zari walitupiana maneno ya kejeli kwenye mitandao ya kijamii baada ya Zari kumualika Diamond kuhudhuria siku ya kuzaliwa ya binti yao, Tiffah.

Video kutoka kwa tafrija hiyo zilimuudhi Shakib ambaye alimsuta Zari kwa kuendekeza hisia kwa Diamond licha ya kuwa tayari walisha achana muda mrefu – 2018.



Zari alikanusha madai hayo akisema kuwa ujio wa Diamond katika tafrija ya siku ya kuzaliwa binti yao ilikuwa jambo la kushtukiza kwani hata yeye mwenyewe hakuwa na taarifa.

Zari alimfokea Shakib kwamba alikuwa ni mtu mwenye mashaka tele katika uhusiano wao, akimtaka kukomaa na kujua kwamba uhusiano wake na Diamond si kitu chochote zaidi ya kushirikiana kuwalea watoto tu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved