logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke Aishi Na Maiti Ya Pasta Wake Nyumbani Kwake Kwa Miezi 2 Akitumai Atafufuka

Mwanamke mmoja amezua kioja katika wilaya ya Iringa nchini Tanzania baada ya kupatikana akiwa na maiti ya mchungaji wa kanisa lake nyumbani kwake, zaidi ya miezi 2 baada ya kufa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani06 December 2024 - 16:32

Muhtasari




     Mwanamke mmoja amezua kioja katika wilaya ya Iringa nchini Tanzania baada ya kupatikana akiwa na maiti ya mchungaji wa kanisa lake nyumbani kwake, zaidi ya miezi 2 baada ya kufa.


    Kwa mujibu wa Ayo TV nchini humo, mwanamke huyo ambaye alikuwa mshirika wa mchungaji huyo alipatikana akiwa amehifadhi mwili wake kwa zaidi ya miezi mbili nyumbani kwake.


    Alipohojiwa na maafisa wa polisi, mwanamke huyo alijieleza kwamba alifanya hivyo si kwa matakwa yake bali kutokana na matakwa ya marehemu kwa waumini wake kabla hajafa.


    Alisema kwamba marehemu mchungaji aliwapa waumini wake masharti makali ya kutoruhusu kuzikwa kwa maiti yake, kwani angefufuka baada ya siku 4 za kufa.


    Hata hivyo, mwanamke huyo aliendelea kuishi na maiti hiyo hata baada ya siku 4 kupita na kutoona dalili zozote za ufufuo wa mchungaji wake.


    Mzee wa kijiji hicho aliambia Ayo TV kwamba pasta huyo alijiunga nao miaka miwili iliyopita akitokea mkoa wa Tanga na akawa anafanya shughuli zake za kuhubiri.


    “Mtu huyu alijiunga nasi Juni 2022 kutoka Tanga na kujitambulisha kuwa ni mhubiri. Alisema alitaka kuanzisha kanisa katika eneo hilo na alipata mahali karibu na kanisa hilo. Tumekuwa tukiishi kwa amani,” alisema kwenye ripoti ya Ayo TV.


    Mzee huyo alieleza kwamba pasta alianza kuugua mwezi Agosti mwaka huu na baadae akapotea bila wao kujua kama alifariki.


    “Agosti mwaka huu alikwenda Mwanza na kurudi akiwa hajisikii vizuri. Alikuwa akikohoa sana na kutema damu. Nilimshauri apate msaada wa matibabu kwenye zahanati, lakini akasema anapata nafuu lakini pia aliahidi kurejea.”


    “Nilikutana naye tena siku tofauti na alikuwa bado hajisikii, hivyo nilimwomba aende hospitali lakini alikataa,” alieleza.


    Hata hivyo, hali yake ilizidi kuwa mbaya, na mwenyekiti akawakusanya wazee wengine wa kijiji, ambao walimshawishi aende hospitali. Msole alieleza kuwa alikaa wiki chache bila kuonana na Mchungaji lakini anaweza kumtuma mwanae kwenda kumchungulia na kumpa chakula.


     “Nilimwomba mwanangu atembelee nyumbani kwa mchungaji na kuwapa chakula na yule mama aliyekuwa akimhudumia Septemba 26. Nilimtuma tena Oktoba lakini muda wote huo hakumuona mhubiri huyo kwani mwanamke huyo angeweza kupokea chakula,” alisimulia.


    Hata hivyo, mkuu wa kijiji alishuku kuwa kuna jambo fulani lisilofaa na akaamua kwenda kumwona mhubiri mwenyewe.


    Alipofika nyumbani alimkuta yule mama ambaye alikuwa anasitasita kumruhusu kuonana na Mchungaji.



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved