logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Mimi Ni Slim Na Light-Skin” MP Peter Salasya Awajibu Wale Wanaofikiria Yeye Ni Mweusi

“Kumbe watu hufikiria mimi ni mu dark skin hehe ni camera tu hunitoa mbaya but am slim and light skin,” Salasya alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani08 December 2024 - 16:25

Muhtasari


  • Watu hao walionyesha furaha na kukutana na Salasya na kueleza jinsi ambavyo wamekuwa wakifikiria muonekano wake.
  • Mmoja alisema kwamba yeye amekuwa akifikiria Salasya ni mtu mweusi mnene kiasi kumbe ni tofauti na yule aliyemuona.



MBUNGE wa Mumias Mashariki, Peter Salasya amewajibu wale ambao hawajawahi kutana naye ana kwa ana na ambao wana taswira tofauti ya muonekano wake vichwani mwao.


Kupitia kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii, Salasya aliweka wazi kwamba kuna baadhi ya watu ambao hawajawahi kutana naye wanafikiria kwamba yeye ni mtu mweusi na pengine mnene.


Alikanusha madai hayo akisema kwamba yeye ni mweupe kwa ngozi na pia ni mwembamba lakini wakati mwingine kamera humtoa kuonekana mweusi hivyo kuwachanganya watu kuusu muonekano wake halisi.


“Kumbe watu hufikiria mimi ni mu dark skin hehe ni camera tu hunitoa mbaya but am slim and light skin,” Salasya alisema.


Mbunge huyo alikuwa akiwaelezea watu waliokutana naye ghafla baada ya kutua jijini Mombasa kwa ajili ya michezo ya wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mombasa iliyoanza Jumamosi.


Watu hao walionyesha furaha na kukutana na Salasya na kueleza jinsi ambavyo wamekuwa wakifikiria muonekano wake.


Mmoja alisema kwamba yeye amekuwa akifikiria Salasya ni mtu mweusi mnene kiasi kumbe ni tofauti na yule aliyemuona.


Mbunge huyo wa DAP-K kwa sasa yuko katika vita vikali na baadhi ya wandani wa chama cha ODM ambapo aliweka wazi lengo lake ni kuhakikisha amemng’oa kiongozi Raila Odinga katika ukanda wa Magharibi kwa kufifisha ushawishi wake.


Salasya alimshtumu Odinga kwa kusaliti Gen Z alipoungana na Ruto wakati Maandamano ya vijana hao yalikuwa yamefika kilele chake kati ya mwezi Juni na Agosti mwaka huu.


“Tumeshaanza kufanya zoezi la kutoa elimu ya kiraia, tukiwaambia watu wetu kutoka Magharibi mwa Kenya Raila Odinga ni nani,” Salasya alifichua.

Mbunge huyo kijana alidai kwamba Odinga tayari ameitisha kikao na wanachama wa Odinga katika kile alisema ni kuanza kuwatishia dhidi ya kutonena kwa sauti moja ya muongozo wa chama.

“Na baada ya kusikia hivyo naambiwa ameita mkutano na wananchama akiwatishia kwa kutumia kamati za bunge. Ningependa kuwaambia watu kutoka Magharibi, wale waheshimiwa wanaoenda kumuona, ni kwamba tu kama hawawezi onyesha mshikamano watatolewa kwenye kamati za bunge,” Salasya alidai.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved