logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Siku Wakenya Wataacha Kuni’support Nitaacha Muziki!” – Rayvanny

Akitoa shukrani zake, Rayvanny alifichua kwamba siku mashabiki wa Kenya watagoma kusapoti muziki wake, basi biashara yake katika muziki itakuwa imefika mwisho.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani09 December 2024 - 10:57

Muhtasari


  • Chapisho lake lilijiri siku moja baada ya vurumai kushuhudiwa katika ukumbi wa Polo ambapo Furaha Fest ilikuwa inafanyika.
  • Willy Paul alionekana kuendeleza chuki hiyo hadi kwa Rayvanny, ambapo alikataa kutumbuiza kolabo yao ya pamoja ya ‘Mmmh’ iliyotoka miaka 5 iliyopita.



NGULI wa muziki kutoka lebo ya muziki ya Next Level Music, Raymond Mwakyusa maarufu kama Rayvanny ameonesha fadhila zake kwa mashabiki wake kutoka Kenya kwa kuendelea kumpa sapoti kubwa.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, alichapisha ujumbe wa kuwashukuru mashabiki wake kutoka Kenya baada ya kujitokeza kwa wingi katika shoo ya Furaha Fest alikokuwa miongoni mwa wasanii waliotumbuiza.


Akitoa shukrani zake, Rayvanny alifichua kwamba siku mashabiki wa Kenya watagoma kusapoti muziki wake, basi biashara yake katika muziki itakuwa imefika mwisho na hatokuwa na budi ila kutafuta kitu kingine cha kufanya mbali na muziki.


“Mimi ni Mtanzania 🇹🇿 Napenda mashabiki Wote wanao support Rayvanny Duniani kote, ila siku wakenya 🇰🇪🇰🇪 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪 wakiacha kusaidia rayikimani yako ni kusaidia rayikimani yako mengi,” Rayvanny alisema.


Chapisho lake lilijiri siku moja baada ya vurumai kushuhudiwa katika ukumbi wa Polo ambapo Furaha Fest ilikuwa inafanyika.


Zogo hilo lilijiri baina ya Willy Paul na uongozi wa Diamond Platnumz ambaye aliishia kuondoka kwa ghadhabu bila kutumbuiza licha ya kuratibiwa kuwa miongoni mwa watumbuizaji.


Willy Paul alionekana kuendeleza chuki hiyo hadi kwa Rayvanny, ambapo alikataa kutumbuiza kolabo yao ya pamoja ya ‘Mmmh’ iliyotoka miaka 5 iliyopita.


DJ alipomchezea Willy Paul wimbo huo wakati anatumbuiza jukwaani, msanii huyo alimfokea na kumtaka kuweka wimbo mwingine, huku akiutaja wimbo huo kama ‘takataka’.


Lakini Rayvanny kwa upande wake alisema kwamba japo Pozee alionyesha dharau kolabo yao, yeye bado anamkubali kama kakake.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved