logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Hii Mimba Yangu Sikununua!” Mammito Afichua Mhusika Wa Ujauzito Wake Ni Nani

"Kwa huyu, ni mtu ambaye si maarufu mitandaoni. Na nafikiri mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa nataka," alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani10 December 2024 - 13:15

Muhtasari


  • “Hii mimba yangu sijanunua, ni ya mtu tu; ni kijana tu wa watu na ni mtoto wa mtu Fulani,” Mammito alieleza.
  • Alisema kwamba kabla ya kuamua kubeba ujauzito, alikuwa anataka mtu ambaye si maarufu mitandaoni na ndiye aliyepata.



MCHEKESHAJI Mammito Eunice kwa mara ya kwanza amenyoosha maelezo kuhusu ukungu unaozingira mhusika wa ujauzito wake.


Akizungumza na Betty Kyalo kwenye runinga ya TV47, Mammito alisema kwamba mimba yake ina mhusika mahsusi kwani hakuinunua.


Mchekeshaji huyo alisisitiza hata hivyo kwamba baba mwanawe mtarajiwa ni mtu na yuko jijini Nairobi lakini akasema hayuko tayari kufichua utambulisho wake.


“Hii mimba yangu sijanunua, ni ya mtu tu; ni kijana tu wa watu na ni mtoto wa mtu Fulani,” Mammito alieleza.


Kuhusu ni kwa nini hayuko tayari kumtambulisha mhusika huyo kwa mashabiki wake mtandaoni, Mammito alisema kuwa anafanya hivyo ili kumkinga yeye na pia mwanawe kutoka kwa hukumu hasi za watu wa mitandaoni.


‘Lazima wafichwe hii Nairobi. Huwezi jua. Useme ndio huyu waseme ooh hakai vizuri na wengine wamchukue na mimi sasa hivi nina umri wa miaka 31, sitaki kuanza kuuliza mtu eti rangi uipendayo ni gani, katika huu umri nimeshakua sasa, unaelewa,” Mammito alifafanua.


Akizungumzia kuhusu uvumi wa kuhusisha mimba yake na mchekeshaji mwenza, Butita Eddy, Mammito alikanusha kwa haraka akisema kwamba yeye na Butita ni mambo ya zamani ambayo ytalifika mwisho takribani miaka 4 iliyopita.


Alisema kwamba kabla ya kuamua kubeba ujauzito, alikuwa anataka mtu ambaye si maarufu mitandaoni na ndiye aliyepata.


“Mimi na Butita ni maneno ya kale, ni muda mrefu uliopita kama miaka 4 iliyopita. Kwa huyu, ni mtu ambaye si maarufu mitandaoni. Na nafikiri mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa nataka, mwenye anajishughulisha na mambo tofauti kabisa na tasnia yetu ya mitandaoni.”


“Kwa sababu awali nimeshawahi kuchumbiana na mtu kwenye tasnia hii na nilichagua kutochumbiana na mtu kutoka hapo tena. Nilichomeka lakini nilijiambia kwamba ningetaka kitu tofauti. Mtu ambaye ananiambia kuhusu kazi yake yenye sielewi,” alisema.


Akizungumzia kuhusu shoo yake inayotarajiwa siku 10 zijazo yenye mada ‘Maandamano Baby’ na ni kwa nini aliipa shoo hiyo jina hilo, Mammito alisema;


“Wakati niligundua kwamba nina mimba nilifurahia na nikajiambia kwamba ni sharti niwataarifu mashabiki wangu kuhusu safari yangu ya ujauzito. Mashabiki wangu wameniona tangu nilipoanza ucheshi nikiwa kama miaka 18 na wameniona nikikua…”


“…na pia nimekuwa nikizungumza kuhusu kuvunjwa moyo na jinsi wanaume wa Nairobi walivyo, lakini sasa nina kitu kipya cha kuzungumza, hivyo nikaona niwataarifu kwa sababu hiki ndicho kitu kikubwa kilichotokea kwangu mwaka huu, sawa na Maandamano yalivyokuwa tukio kubwa, hivyo nikaona kuuunganisha vitu hivyo viwili litakuwa jambo zuri.”


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved