logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msaani Harmonize atoa onyo kabla ya tamasha lake nchini Uganda.

Msaani wa nyimbio za bongo Harmonize ametoa onyo kali kwa wasaani wa Uganda kabla ya tamasha lake

image
na OTIENO TONNY

Burudani16 December 2024 - 10:09

Muhtasari


  • Harmonize aahidi kudumisha amani wakati wa tamasha lake nchini Uganda.
  • Kauli ya Harmonize inakuja huku kukiwa na mvutano unaoongezeka katika tasnia ya muziki Afrika Mashariki
caption

Msaani wa bongo Harmonize ametoa onyo kali kwa wasaani wa Uganda dhidi ya kuvuruga tamasha lake litakalofanyika nchini humo. Hii ni baada ya Diamond kubishana na Willy Paul wakati wa tamasha  ya Furaha Fest nchini Kenya.

Harmonize amesems kwamba atahakikisha kuwa tamasha hilo nchini Uganda litakuwa lenye mafanikio bila vurugu ya aina yoyote akisema kuwa hatakubali vurugu kutokea akiahidi kukabiliana na msaani yeyote atakaye jaribu kuzua sintofahamu. Harmonize alidokeza  haya akirejelea tokeo lililotokea nchini Kenya hivi majuzi wakati Diamond Platnumz alikosa kutumbuiza mashabiki akikiri ukosefu wa usalama.

Tukio hilo lilifichua malalamiko yanayoendelea kuhusu kutokuwa na usawa katika tasnia ya usanii hasa wasanii wa Kenya na Tanzania, huku Willy Paul akiwatuhumu waandalizi wa tamashi hilo kuwapendelea wasanii wa Tanzania.

Diamond Platnumz alikanusha madai hayo, akihimiza umoja na kufanya kazi kwa bidii badala ya kuchochea migawanyiko. Alisema kuwa tendo la Willy Paul lilisukumwa na kiu ya kutafuta kiki na umarufu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved