logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mulamwah: Nilianza Ku’save 3k Kila Siku Desemba Mwaka Jana, Sasa Nina Jumla Ya Ksh 1.1m

Baada ya kuvunja kibubu chake, Mulamwah alisema kwamba shilingi elfu 3 yake ya kila siku imezalisha jumla ya milioni 1.1 baada ya mwaka.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani16 December 2024 - 15:43

Muhtasari


  • “Uliwezaje kupata kazi ambayo unaweza kuwekeza 3k kila siku?” shabiki mmoja alimuuliza.
  • “Tunavumilia tu matusi huku online tukijua tunachotaka,” Mulamwah alijibu.



Mchekeshaji na mtangazaji wa redio, Kendrick Mulamwah amefichua jumla ya pesa ambazo amekuwa akiwekeza kidogo kidogo kwa kipindi cha mwaka mmoja.


Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Mulamwah alifichulia mashabiki wake kwamba alianza safari ya kutenga shilingi elfu 3 kila siku Desemba 15 mwaka jana na mwaka mmoja baadae amevunja kibubu.


Baada ya kuvunja kibubu chake, Mulamwah alisema kwamba shilingi elfu 3 yake ya kila siku imezalisha jumla ya milioni 1.1 baada ya mwaka.


“God is great - 3k per day savings Challenge imekamilika kwa 2024. 💪🔥 ilianza tarehe 15 Desemba mwaka jana kuweka pole pole tu. Umeweka ngapi? kama hujaweka tuanze wote for next year,” Mulamwah alisema.



Mulamwah alitumia fursa hiyo kuwashauri mashabiki wake kuwa na hulka ya kuwekeza hela kidogo kidogo akisema kuwa hiyo ndio njia pekee ya kujisaidia.


Alisema kwamba hizo hela zake sasa ataongeza shamba.


“Haijalishi ni kiasi gani ata 20, 50, 100, 1k kwa siku ni sawa. Jaribu kuweka pesa kwa sababu itakuokoa kila wakati. Wacha tuongeze kaploti sasa,” Mulamwah alisema.


Hata hivyo, kilichowashangaza wengi ni kauli yake kwamba amekuwa akiwekeza shilingi elfu 3 kwa kila siku kwa mwaka mzima.


Mmoja alimuuliza ni kazi gani hiyo alipata ya kumwezesha ku’save 3k kila siku na Mulamwah alijibu akisema kwamba ni kazi za mtandaoni huku akimtaka kujiunga naye kwa mafunzo jinsi ya kutengeneza hela kiasi hicho na zaidi kwa siku.


“Uliwezaje kupata kazi ambayo unaweza kuwekeza 3k kila siku?” shabiki mmoja alimuuliza.


“Tunavumilia tu matusi huku online tukijua tunachotaka,” Mulamwah alijibu.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved