logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Hata Sijawahi Kuwa Na 10k Subscribers” Gidi Akanusha Kupoteza Wafuasi YouTube

Taarifa ambazo zimekuwa zikisambaa baada ya Gidi kutumbuiza katika sherehe za Jamhuri ni kwamba alipoteza wafuasi zaidi ya 10k YouTube saa chache baada ya sherehe hizo kukamilika.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani18 December 2024 - 14:42

Muhtasari


  • Gidi alikanusa uvumi huo akisema kwamba hata chaneli yake ya YouTubew haijawahi fikisha wafuasi 10, achia mbali kuwapoteza wafuasi hao.
  • Sherehe za Jamhuri zilifanyika jijini Nairobi katika uwanja wa Uhuru Gardens ambapo Gidi alikuwa miongoni mwa wasanii wakongwe waliotumbuiza kuadhimisha miaka 61 ya Kenya kujitawala.



MTANGAZAJI wa Radio Jambo, Joe Gidi amekanusha madai yanayoenezwa mitandaoni kwamba alipoteza wafuasi wengi kwenye jukwaa la YouTube baada ya kutumbuiza katika sherehe za Jamhuri, Desermba 12.


Akizungumzia uvumi huo kwa mara ya kwanza kupitia ukurasa wake wa Facebook, Gidi alisema kwamba taarifa hizo hazima mashiko na kuzitaja kama porojo zinazoendeshwa na wanablogu kutafuta kiki tu mtandaoni.


Taarifa ambazo zimekuwa zikisambaa baada ya Gidi kutumbuiza katika sherehe za Jamhuri ni kwamba alipoteza wafuasi zaidi ya 10k YouTube saa chache baada ya sherehe hizo kukamilika.


Gidi alikanusa uvumi huo akisema kwamba hata chaneli yake ya YouTubew haijawahi fikisha wafuasi 10, achia mbali kuwapoteza wafuasi hao.


Alisema kwamba yeye hajawahi tyumia kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii kutengeneza pesa, akisisitiza kwamba huitumia tu kujivinjari na pia akaweka wazi kuwa yeye mara nyingi hutumia mtandao wa Facebook.


“Nimeona baadhi ya TikTokers na wanablogu wakitumia hadithi hii bandia kwenye maoni yao. Situmiki kwenye YouTube na sijawahi kuwa na wafuasi 10k. Sipokei mapato ya mitandao ya kijamii, ninaitumia tu kwa maoni ya kijamii. Ninafanya kazi kwenye facebook pekee. Jihadhari na kupuuza habari ghushi zinazoundwa na watu wanaotafuta kupenda na ubofye chambo mtandaoni,” alisema.


Sherehe za Jamhuri zilifanyika jijini Nairobi katika uwanja wa Uhuru Gardens ambapo Gidi alikuwa miongoni mwa wasanii wakongwe waliotumbuiza kuadhimisha miaka 61 ya Kenya kujitawala.


Pindi tu ilipobainika kwamba mtangazaji huyo maarufu wa kipindi cha Patanisho alikuwa kwenye orodha ya watumbuizaji wakongwe, Wakenya haswa kwenye mtandao wa X walianzisha kampeni za kumshambulia na wengine hata kumtumia jumbe zisizofurahisha kwenye simu yake.


Hata hivyo, Gidi alionekana kutoyumbishwa na mashambulizi hayo ambayo siku ya Jamhuri alitoa moja la tumbuizo la kuvutia akiwa na mwenzake, MajiMaji ambaye walikuwa wanaimba naye.


Kabla ya kujizolea umaarufu kama mtangazaji kwenye Radio Jambo, Gidi alikuwa msanii wa kibabe mapema miaka ya 2000s akiwa na MajiMaji ambapo miongoni mwa vibao vyao vingi, ‘Unbwogable’kinasalia kuwa kibao kilichowatambulisha zaidi kwa Wakenya wa matabaka mbalimbali.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved