logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maandy Ataka Vita Ya Maneno Kati Ya Wasanii Wa Gengetone Na Arbantone Kukomeshwa

Maandy anahisi kwamba muziki wowote uwe Gengetone au Arbantone ni mzuri tu ukifanywa vizuri haijalishi na nani, na kuwataka wasanii hao kushirikiana badala ya kusutana.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani08 January 2025 - 10:02

Muhtasari


  • Hata hivyo, mzozo huo umeonekana kumchukiza Maandy ambaye amewataka wasanii kutoka pande hizo mbili kuheshimiana na kushirikiana badala ya kuanzisha vita vya kibabe.
  • Kauli yake inajiri siku mbili tu baada ya kushuhudiwa kutupiana maneno baina ya DJ wa Gengetone VDJ Jones na msanii wa arbantone, YBW Smith 



MSANII wa kizazi kipya, Maandy amekuwa wa hivi punde kutoa tamko kuhusu vita vya maneno kati ya wasanii wa Gengetone na wale wa Arbantone.


Mzozo huo uliibuka pindi tu kikundi cha Gengetone, Ethic Entertainment walipotangaza wiki jana kwamba wangerudi pamoja kufanya muziki, miezi kadhaa baada ya kutengana.


Ujio wao ulivutia vita vya maneno kutoka kwa wenzao wa Arbantone, baadhi wakionekana kukejeli ujio huo huku wengine wakiwaunga mkono kwa kufanya uamuzi wa kurudi pamoja.


Hata hivyo, mzozo huo umeonekana kumchukiza Maandy ambaye amewataka wasanii kutoka pande hizo mbili kuheshimiana na kushirikiana badala ya kuanzisha vita vya kibabe.


Maandy anahisi kwamba muziki wowote uwe Gengetone au Arbantone ni mzuri tu ukifanywa vizuri haijalishi na nani, na kuwataka wasanii hao kushirikiana badala ya kusutana.


“Tunaweza komesha kabisa aya yote ya sijui ni nani amerudi, ni nani ameenda, ni nani amefanya au ameimba…tunaweza ishi vizuri pamoja sisi wote. Kama hauhisi kutishiwa, haufai kuingilia hayo mambo. Muziki ni muziki tu bora ni noma,” Maandy alishauri kupitia Instagram.


Kauli yake inajiri siku mbili tu baada ya kushuhudiwa kutupiana maneno baina ya DJ wa Gengetone VDJ Jones na msanii wa arbantone, YBW Smith kuhusu ni muziki upi bora kati ya gengetone na arbantone.


Baada ya Ethic kurudi na kuachia wimbo huo, hizi hapa ni baadhi ya kuali kutoka kwa wasanii wa Arbantone;


“Napata DMs kwamba Gengetone imerudi, labda hawa wagenge wastone. Shindano la 1v1 likuje basi,” YBW Smith aliandika.


“Sikatai wamerudi, lakini watawezana na mimi kweli,” Tipsygee aliuliza.


“Heshima kwa wasanii wa gengetone lakini mistari kwa mistari hakuna anayeniweza,” alisema Sosa the prodigy.


‘Kusema ukweli mimi ninahisi kama gengetone itafufuka, litakuwa ni jambo zuri zaidi. Najaribu kutafakari tamasha la gengetone dhidi ya arbantone. Na kwa kuongezea, arbantone tunahitaji huu ujio wa gengetone ili kuimarika zaidi,” Sean MMG alisema.


 


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved