logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Stevo Simple Boy: Kwa Nini Siwezi Kubali Mpenzi Wangu Kuja ‘Sleepover’

Alipoulizwa ni lini mara ya miwsho alishiriki mapenzi, Stevo alijibu kwa utani akisema, “Ni kitambo sana, siwezi sema” na kusisitisha kwamba yeye kula tunda ni hadi siku ya ndoa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani09 January 2025 - 11:03

Muhtasari


  • Simple alisisitiza kwamba hawezi mkubalia mrembo kuja kwake kulala naye akisema kwamba, “shida iko, kwa sababu kuna majaribu. Naweza jikuta nimefanya mambo ambayo hayafai.”



MSANII STEVO SIMPLE BOY amefunguka kuhusu mipango yake kuelekea siku ya wapendanao ambayo itaadhimishwa mwezi ujao, Februari 14.


Katika mahojiano na Trudy Kitui, Stevo Simple Boy alisema kwamba tofauti yake na watu wengi, haamini katika mapenzi ya mwanamume na mwanamke bila kuoana rasmi.


Akitetea msimamo wake, Stevo alisema kwamba mapenzi ya bila kuoana yanaweza isha wakati wowote tu shida inapotokea, tofauti na ndoa ambayo itadumu kwa muda baina ya mawimbi.


“Unajua tofauti yangu na wengine, kuna boyfriend na girlfriend halafu kuna ndoa. Hivyo vitu ni tofauti sana, mimi huwa naangalia ndoa kwa sababu unajua girlfriend atakuja ‘ooh Stevo nakupenda...’ halafu anasepa. Lakini mke anafaa apende mtu wake kwa hali zote,” Stevo alisema.


Rapa huyo alisema kwamba nyakati za sasa kimapenzi ni tofauti na zamani, japo alikubaliana na dhana kwamba kabla wapenzi wawe wanandoa, ni sharti waanze kama girlfriend na boyfriend.


Stevo alisema kwamba vijana wa siku hizi wanaanza kualikana kwa ‘sleepover’ hata kabla ya kila mmoja kujua nyumbani kwa mpenzi wake.


“Ukiangalia mambo ya kitambo na siku hizi ni tofauti. Kama ni msichana anapenda mwanaume ama mwanamume anapenda msichana, anafaa ampeleke kwao familia imuone na kumjua. Lakini haya mambo ya Sleepover hapana. Hayako kwa Biblia,” Stevo alisema.


“Mimi huwa sileti msichana kwangu kwa sleepover kwa sababu hiyo haiko kwa Biblia.  Kwa uelewa wangu, kama ni yule mrembo ambaye hatujajuana vizuri na anataka kuja kunitembelea, akuje tu mchana anione na apange nyumba na jioni ikifika aende kwake,” Stevo aliongeza.


Simple alisisitiza kwamba hawezi mkubalia mrembo kuja kwake kulala naye akisema kwamba, “shida iko, kwa sababu kuna majaribu. Naweza jikuta nimefanya mambo ambayo hayafai.”


Alipoulizwa ni lini mara ya miwsho alishiriki mapenzi, Stevo alijibu kwa utani akisema, “Ni kitambo sana, siwezi sema” na kusisitisha kwamba yeye kula tunda ni hadi siku ya ndoa.


Msanii huyo alifichua kwamba mwaka jana alipata mpenzi wakapendana lakini kwa bahati mbaya mambo yakaenda mrama na hivyo akaamua anatulia hadi pale atakapompata anayemfaa.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved