logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Nitamuita Furaha”: Harmonize Aomba Mungu Kumjaalia Mtoto Wa Kike 2025

Licha ya kutendwa kimapenzi mara kadhaa, Harmonize yuko mbioni tena kujaribu karata tata katika uwanja wa mapenzi, safari hii akiwa na tumaini la kutoka na mtoto wa kike, na si mikono mitupu.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani10 January 2025 - 13:11

Muhtasari


  • Hata hivyo, Harmonize hakuweza kubainisha ni jinsi gani atapata mtoto huyo bila ya kuwa na mpenzi, lakini kama wanavyosema, penye nia pana njia.
  • Msanii huyo hajakuwa na bahati kimapenzi kwani amekuwa akiingia na kutoka katika mapenzi licha ya kuonekana kujitutumua.



BOSI WA LEBO ya Konde Music Worldwide, Harmonize amefichua kwamba ombi lake mwaka huu ni kuongeza mtoto mwingine.


Msanii huyo ambaye ni baba kwa binti mmoja kwa jina Zuhu, alifichua kwamba angependa kuongeza mtoto mwingine wa kike mwaka huu ili kuwa ndugu mdogo kwa binti wa kwanza.


Alisema kwamba iwapo atapata mtoto huyo, atampa jina ‘Furaha’ kuashiria furaha aliyo nayo kuwa baba kwa mara nyingine tena.


Harmonize amekuwa akijishebedua na watoto wawili wa kike, Zuhu na binti wa mpenzi wake wa zamani wa Poshy Queen kwa jina Nova ambaye anampenda licha ya kuachana na mamake miezi michache iliyopita.


Harmonize alifunguka kwamba mabinti zake Zuhu na Nova sasa wanafaa kujiweka tayari kwa binti yao mwingine ajaye, Furaha.


“Ombi langu Mungu baba, natamani sana nipate mtoto wa kike 2025. Mitamuita Furaha. Zureha na Nova tunakungoja wewe Furaha,” Harmonize aliandika.


Hata hivyo, Harmonize hakuweza kubainisha ni jinsi gani atapata mtoto huyo bila ya kuwa na mpenzi, lakini kama wanavyosema, penye nia pana njia.


Msanii huyo hajakuwa na bahati kimapenzi kwani amekuwa akiingia na kutoka katika mapenzi licha ya kuonekana kujitutumua.


Alianza mapenzi na Wolper ambaye ameachana juzi na mume wake wa ndoa, Rich Mitindo kabla ya kumpenda raia wa Italia Sarah Mitchelotti na baadae Kajala Masanja mara mbili, lakini hakuna penzi lililodumu.


Mwaka jana, alitangaza kuingia katika huba na mrembo Poshy Queen ambaye licha ya kuongozana naye hadi kanisani na kufananisha nguo, penzi hilo halikuweza kuona mwishoni mwa mwaka kwani lilisambaratika vipande vipande.


Licha ya kutendwa kimapenzi mara kadhaa, Harmonize yuko mbioni tena kujaribu karata tata katika uwanja wa mapenzi, safari hii akiwa na tumaini la kutoka na mtoto wa kike, na si mikono mitupu.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved