logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shule Ya Mang’u Kusafirisha Zawadi Yao Ya Ndege Kutoka JKIA Kupitia Thika Road

Ndege hiyo aina ya Boeing 737-700 itasafirishwa Jumapili ya Januari 12 kutoka uwanja wa JKIA kupitia barabara ya Eastern Bypass, Thika Road hadi shuleni Mang’u.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani12 January 2025 - 12:00

Muhtasari


    BAADA ya miezi kadhaa ya kupanga kuhusuc usafiri wa zawadi yao adimu, shule ya upili ya kitaifa ya Mang’u hatimaye imepata njia mwafaka ya kusafirisha zawadi ya ndege waliyopewa na shirika la ndege la KQ hadi shuleni mwao.


    Shirika la ndege la Kenya Airways (KQ) limekabidhi ndege aina ya Boeing 737-700 kwa Shule ya Upili ya Mang’u miezi kadhaa baada ya kutangaza kuwapa zawadi hiyo kama njia moja ya kuwatia motisha wanafunzi lakini pia kuwasaidia katika mafunzo.


    KQ katika taarifa ilisema hatua hiyo ni ya kuhamasisha kizazi kijacho cha wafanyikazi wa anga.


    Ndege hiyo aina ya Boeing 737-700 itasafirishwa Jumapili ya Januari 12 kutoka uwanja wa JKIA kupitia barabara ya Eastern Bypass, Thika Road hadi shuleni Mang’u.


    "Tunaweka historia kwa mchango wa Boeing 737 kwa Shule ya Upili ya Mangu, ili kuhamasisha kizazi kijacho cha wasafiri wa anga!" shirika la ndege lilisema.


    Ndege hiyo ilipokelewa na mkuu wa shule hiyo, John Kuria, ambaye alibainisha kuwa mchakato wa kupata ndege hiyo ulianza zaidi ya miaka mitatu iliyopita.


    Kuria alisema ndege hiyo inakwenda kukuza masomo ya usafiri wa anga katika shule hiyo, na wanafunzi pia watapata mafunzo kuhusu soko la anga la Kenya na kimataifa.


    “Tuna furaha kupokea ndege hii kutoka kwa shirika la ndege la Kenya Airways. Ni safari iliyoanza miaka mitatu iliyopita… na leo mimi ni mtu mwenye furaha. Ni zawadi pia kwangu kwa kadiri taaluma yangu ya ualimu inavyohusika."


    "Ndege hii itakuza masomo ya usafiri wa anga, na tutawafunza vijana hawa kuhusu soko la Kenya na kimataifa katika masuala ya anga," Mkuu wa Shule alisema.


    Makabidhiano hayo yanajiri mwaka mmoja baada ya Waziri wa Barabara na Uchukuzi Kipchumba Murkomen kukabidhi ndege ya shirika la ndege la Kenya Airways kwa Shule ya Upili ya Mang'u.


    Murkomen alisema ndege hiyo itakuwa msaada mkubwa kwa mtaala mpya wa elimu, CBC.


    Aliendelea kusema kuwa ndege hiyo itasaidia mfano wa dhana za vitendo kwa wanafunzi wanaotaka kufuata njia zinazohusiana na urubani.


    "Mchango wa ndege hii, Boeing B737-700, ni kitendo cha heshima na uthibitisho wa KQ kuunga mkono Mtaala unaozingatia Umahiri (pia unajulikana kama CBC) ambao unalenga kusisitiza maslahi ya wanafunzi katika maeneo fulani ya masomo, kutumia ujuzi wao. vipaji vya kuzaliwa, na kubadilisha mapenzi yao kuwa kazi," alisema.



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved