logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Tiktokers Walinishikilia Kama Familia, Sikuwahi Kosa Chakula Na Dawa!” – Rachael Otuoma

Rachael alisema kwamba mwaka huu ndio wangetiiza miaka 10 ya ndoa na Ezekiel Otuoma, huku akimtaja kama mwanamume aliyempa heshima ambayo wanawake wengi hawapati maishani.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani12 January 2025 - 11:19

Muhtasari


  • “Nitaendelea kumpenda huyu mwanamume hata kama ako hapa chini, huyu mwanamume alinipa heshima yenye wanawake wengine hata hampati hapo nje" 

TIKTOKER Rachel Otuoma amewashukuru wanajamii ya TikTok kwa kusimama naye katika takribani kipindi cha miaka 5 ya ugonjwa wa marehemu mumewe, mwanasoka Ezekiel Otuoma.


Mrembo huyo alizungumza kwa ujasiri wakati wa mazishi ya mumewe Jumamosi Janauri 11 katika kaunti ya Siaya na kuwashukuru TikTokers kwa kusimama naye kuhakikisha Otuoma hakuwahi kosa dawa wala chakula katika kipindi chote cha ugonjwa wake.


“Ningependa kushukuru kila mtu, na haswa familia yangu ya TikTok, wueh! Nyinyi watu mmenishikilia kama Otuoma yuko, mmenishikilia kama sasa hivi vile hayuko… tiktokers, ahsante za dhati kwenu,” Rachael alishukuru.


“Ningekosa hata dawa, nilikuwa naenda hapo kwa hiyo TikTok, nitachambwa lakini kuna mmoja atajiotokeza anunue dawa. Hivyo TikTok ni familia yangu. Sikuwahi kosa hata chakula, kama niko hapo TikTok. Otuoma alikuwa anwafinyia jicho, anawatabasamia na mlikuwa mnafurahia, hivyo kwangu TikTok ni familia kubwa sana,” alisema.


Rachael alisema kwamba mwaka huu ndio wangetiiza miaka 10 ya ndoa na Ezekiel Otuoma, huku akimtaja kama mwanamume aliyempa heshima ambayo wanawake wengi hawapati maishani.


“Mkiangalia, hapa si kwamba ninamzika mume wangu kumsahau, hii ni kama kumbukumbu ya 10 ya ndoa yetu. Huu mwaka tungeadhimisha miaka 10. Mkiniangalia hivi mimi ni mwanamke mkakamavu sana. Hakuna kitu kingine kinaweza nitingisha juu ya huyu mwanamume.”


“Nitaendelea kumpenda huyu mwanamume hata kama ako hapa chini, huyu mwanamume alinipa heshima yenye wanawake wengine hata hampati hapo nje. Na bado nitampa hiyo heshima hata kama hayuko nando yangu,” Rachel aliomboleza Ezekiel Otuoma.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved