logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Sisi Hao Tumefika, Kenya Mambo Mbaya!” Polisi 217 Waimba Baada Ya Kutua Haiti

Maafisa hao 217 waliagwa na waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen kuelekea Haiti kuongeza nguvu na wenzao zaidi ya 400 walioondoka nchini mwaka jana.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani20 January 2025 - 09:53

Muhtasari


WIKENDI iliyopita, maafisa 217 zaidi wa Kenya walisafiri kwenda Haito kujumuika na wenzao katika kuleta utulivu katika mitaa ya mji mkuu wa Port-au-Prince.


Katika video iliyoenezwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kufika kwao, maafisa hao walionekana kuwatia moyo wananchi wa taifa hilo la Carrebian kwa nyimbo za kishujaa.


Polisi hao waliimba wakitangaza ubabe wa Kenya katika kulinda amani wakisema Kenya ni mambo mbaya.


“Sisi hao tumefika, Kenya mambo mbaya tena sana,” polisi hao waliimba kwa sehemu.


Maafisa hao 217 waliagwa na waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen kuelekea Haiti kuongeza nguvu na wenzao zaidi ya 400 walioondoka nchini mwaka jana.


“Niliagana na kikosi cha pili cha maafisa wa polisi wa Kenya kwenye Misheni ya Kimataifa ya Usaidizi wa Usalama (MSS) nchini Haiti. Maafisa hao 217 wataimarisha kundi la kwanza la 400 waliotumwa mwaka jana katika taifa hilo la Karibea kurejesha amani,” Waziri Murkomen alisema kupitia X.


Ujumbe huo unaoongozwa na Kenya umepata mafanikio makubwa katika kupunguza ghasia za magenge, na kujipatia sifa kote ulimwenguni, ikiwa ni pamoja na tawala zinazotoka na zinazokuja za Marekani, waziri huyo alifichua.


“Kujitolea kwetu kwa dhamira hii ya kihistoria ni thabiti na tutaendelea kuhamasisha usaidizi wote muhimu wa kimataifa ili kufanikiwa,” Murkomen aliongeza.


Baada ya kutua nchini Haiti, Wanajeshi wa ziada katika Misheni ya Kimataifa ya Usaidizi wa Usalama (MSS) walipokelewa na Waziri Mkuu Alix Didier Fils-Aime na maafisa wengine wa serikali.


Waziri Mkuu alipongeza uimarishaji huo kama hatua muhimu katika kurejesha utulivu nchini.


Kikosi hicho kiliandamana na Naibu Mshauri wa Usalama wa Kitaifa Bw. Joseph Boinnet, Naibu Inspekta Mkuu wa Huduma ya Polisi ya Utawala, Bw. Gilbert Masengeli, na Kamanda Mkuu wa Kitengo cha Huduma, Bw. Ranson Lolmodooni.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved