logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gwiji Wa Muziki Wa Nigeria 2Baba Athibitisha Kuachana Na Mkewe, Annie Macaulay

Kuachana kwao kunajiri siku chache tu baada ya kutolewa kwa msimu wa tatu wa filamu ya Netflix Young, Famous & African

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani27 January 2025 - 10:54

Muhtasari


  • Hata hivyo, baadhi walihisi kwamba taarifa hiyo si ya kweli na kudai akaunti yake ilidukuliwa.
  • Katika sasisho, Idibia amekiri binafsi kuchapisha tangazo hilo kuhusu kutengana kwake na kuachana na mkewe, Annie Idibia.



GWIJI wa muziki wa Nigeria, Innocent Idibia, maarufu kwa jina la 2Baba, ametangaza kuwa yeye na mkewe Annie Macaulay wametengana na kwa sasa wamewasilisha kesi ya talaka.


2Baba alitumia akaunti yake ya Instagram siku ya Jumapili kushiriki habari hizo na mashabiki wake.


Aliandika, "Habari kwa watu wangu wazuri wa mashirikisho yote. Kweli, jambo hili ninalopaswa kusema ni fupi lakini pia refu…Mimi na Annie Macaulay tumetengana kwa muda sasa, na kwa sasa tumewasilisha kesi ya talaka.”


"Nitatoa taarifa kwa vyombo vya habari hivi karibuni ili kusema hadithi yangu. Sio kwa sababu ni haki ya mtu yeyote kujua kuhusu maisha yangu binafsi lakini kwa sababu ninawapenda watu wangu na ninahitaji wajue kutokuwa na hatia au kosa langu. Endelea kubarikiwa watu wangu. Nawapenda nyote.”


Kumbuka ndoa yao imekumbwa na uvumi wa talaka baada ya Annie kumshtaki 2Baba kwa kutokuwa mwaminifu.


Hata hivyo, baadhi walihisi kwamba taarifa hiyo si ya kweli na kudai akaunti yake ilidukuliwa.


Katika sasisho, Idibia amekiri binafsi kuchapisha tangazo hilo kuhusu kutengana kwake na kuachana na mkewe, Annie Idibia.


Katika video iliyoshirikiwa kupitia hadithi yake ya Instagram siku ya Jumapili, mwimbaji huyo alizungumzia mzozo huo, akisema, "Ndio, wabariki watu wangu wote. Hakuna mtu aliyedukua akaunti yangu.”


Ufichuzi huu umekuja baada ya mitandao ya kijamii kuzua tafrani wakati ujumbe wa Instagram kutoka kwa akaunti iliyothibitishwa ya 2Baba ulitangaza kutengana kwa wanandoa hao.


Chapisho hilo lilisomeka, “Sawa, jambo hili ninalopaswa kusema ni fupi lakini pia refu. Mimi na Annie Macaulay tumetengana kwa muda sasa na kwa sasa tumeomba talaka. Ningetoa taarifa kwa vyombo vya habari hivi karibuni ili kusema hadithi yangu, si kwa sababu ni haki ya mtu yeyote kujua kuhusu maisha yangu ya kibinafsi, lakini kwa sababu ninawapenda watu wangu na ninahitaji wajue kutokuwa na hatia au kosa langu. Endelea kubarikiwa, watu wangu. Ninawapenda nyote.”


Muda mfupi baadaye, chapisho lingine lilitokea kwenye akaunti hiyo, likidai kuwa lilikuwa limedukuliwa. "Akaunti yangu ya Instagram imedukuliwa, juhudi zinafanywa kuchukua udhibiti," chapisho hilo lilisomeka.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved