logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vera Sidika, Chimano, Skillo Wapigiwa Debe Kujiunga Na YFA Ya Netflix

"Vera angeonekana mzuri kwenye onyesho letu. Ninahisi kama yeye ni mrembo, analeta nyash yote, na ninahisi kama anaweza kurusha miguno. Vera," Zari alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani28 January 2025 - 10:35

Muhtasari




    WIKI chache baada ya Netfix kuachia msimu wa tatu wa filamu ya uhalisia, Young Famous & African, Wakenya mbalimbali wamejitokeza na kuonyesha kutoridhishwa kwao jinsi hakuna Mkenya hata mmoja amefanikiwa kujumuishwa tangu mswimu wa kwanza mwaka 2022.


    Malalamiko haya yametoka si tu kwa Wakenya wa kawaida pekee lakini pia maceleb mbali mbali ambao wamesimama kidete kuwapigia debe maceleb wenzao ambao wanaona wana vigezo sawa na wale waliojumuishwa kwenye kipindi hicho cha Netflix.


    Siku chache zilizopita, mmoja wa mastaa kwenye kipindi hicho, mfanyibiashara Zari Hassan alikuwa humu nchini ambapo alikuwa mtu wa kwanza kutoa maoni kuhusu ni Mkenya yupi anayestahili kwenye Young, Famous & African.


    Zari alimpigia upato mwanasosholaiti Vera Sidika kujumuishwa kwenye msimu ujao, akisema kuwa anastahili pamoja na mvuto wake kwenye mitandao ya kijamii na pia umbile lake la kipekee.


    "Vera angeonekana mzuri kwenye onyesho letu. Ninahisi kama yeye ni mrembo, analeta nyash yote, na ninahisi kama anaweza kurusha miguno. Vera, anafanana na sisi," Zari alisema.


    Ungamo la Zari kuhusu Vera lilifungulia mirija ya maoni kutoka kwa maceleb wengine wa Kenya ambapo, Chiki Kuruka, mke na meneja wa msanii Bien naye alitoa maoni akimpendekeza msanii Chimano Willis kama karata bora ya kuwakilisha Kenya kwenye YFA.


    Kwa mujibu wa Kuruka, Chimano ana kila kigezo cha kugeuza vichwa mara mbili mbili kwenye kipindi hicho cha uhalisia kwa fasheni yake ya kipekee.


    “Mpendwa @youngfamousandafrican Kipindi chako ni CHA AJABU! Kitu pekee ambacho kingeifanya kuwa bora zaidi, itakuwa uwepo wa @willis.chimano Tafadhali zingatia! Kutoka kwa shabiki mwenye shauku,” Chiki aliandika kwenye chapisho lake.


    Kama hiyo haitoshi, msanii wa kundi la Wakadinali, Scar Mkadinali naye hakuachwa nyuma kwa maoni yake kuhusu Mkenya anayehisi anastahili kupewa nafasi kujumuika na mastaa wengine wa Kiafrika kwenye YFA.


    Scar Mkadinali alimpendekeza rapa mwenzake, Skillo, akisema ndiye chaguo bora atakayeonyesha ubora wa kiuhalisia wa tamaduni za Wakenya.


    “Wapendwa Young Famous & African, kipindi chenu ni cha ajabu! Kitu pekee ambacho kitafanya kipindi kuwa bora zaidi ni kumuongeza Skillo. Kutoka kwa Rong Rende tunawapa Skillo,” Scar alipendekeza.


    Skillo Kenyan ni rapa wa Kenya, anayejulikana kwa muziki wake wa hip-hop, mara nyingi akitumia "@loskiskillo" kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii kama Instagram; anachukuliwa kuwa msanii anayechipukia katika tasnia ya muziki ya Kenya, haswa katika jamii ya Wajaluo.


    Makala Zinazohusiana


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved