logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Runinga Ya KBC Yatoa Taarifa Baada Ya Ukurasa Wao Wa X Kudukuliwa

KBC iliomba samahani kwa mashabiki wao kutokana na machapisho ambayo yaliyochapishwa kwenye ukurasa huo, wakitoa tahadhari kuu kwamba hayatoki kwao.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani01 February 2025 - 13:34

Muhtasari


  • Hii si mara ya kwanza kwa wadukuzi kuteka kurasa za mashirika na idhaa mbalimbali humu nchini.
  • Mwaka jana, klabu ya soka ya KCB inayoshiriki ligi kuu ya humu nchini, FKF-PL walitangaza kudukuliwa kwa ukurasa wao wa Facebook.



RUNINGA ya shirika la Habari la taifa, KBC imethibitisha kwamba ukurasa wao wa mtandao wa  uko mikononi mwa wadukuzi, saa chache baada ya watumizi wa X kutilia shaka machapisho yao.


Katika taarifa kwenye ukurasa wao wa Facebook, KBC walisema kwamba ukurasa wao wa X umedukuliwa na kufichua kwamba juhudi za kuurudisha mikononi mwao zinaendelea.


KBC iliomba samahani kwa mashabiki wao kutokana na machapisho ambayo yaliyochapishwa kwenye ukurasa huo, wakitoa tahadhari kuu kwamba hayatoki kwao.


“Tahadhari: ukurasa wa KBC Channel 1 kweny X umedukuliwa na tuko katika mchakato wa kuurudisha mikononi mwetu.  Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote na tunatoa ushauri wa watu kuwa makini wanapotangamana na ukurasa huo haswa machapisho ya hivi majuzi,” walisema huku wakiwataka mashabiki wao kufuatilia Habari zao kupitia ukurasa wa Facebook.


Hii si mara ya kwanza kwa wadukuzi kuteka kurasa za mashirika na idhaa mbalimbali humu nchini.


Mwaka jana, klabu ya soka ya KCB inayoshiriki ligi kuu ya humu nchini, FKF-PL walitangaza kudukuliwa kwa ukurasa wao wa Facebook.


Tangazo hilo lilijiri miezi kadhaa baada ya klabu nyingin, Shabana FC pia kutangaza kudukuliwa kwa ukurasa wao wa Facebook.


Chuo kikuu cha Kabarak pia hakikusazwa katika udukuzi huo ambapo walipoteza ukurasa wao wa Facebook kwa siku kadhaa kabla ya kufanikiwa kuurudisha mikononi mwao.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved