logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mumewe Zari Afichua Sababu Ya Kujitambulisha Kwa Kiganda Kwenye YFA Ya Netflix

Ameelezea kwamba alichokifanya wakati wa kujitambulisha kwenye Young Famous & African hakikutokea kwa bahati mbaya

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani02 February 2025 - 08:31

Muhtasari


  • Shakib, ambaye kwa mara ya kwanza katika Maisha yake alitimiza ndoto ya kuonekana kwenye filamu ya Netflix – Young Famous & African,
  • Zari pia aliwafunga midomo baadhi ya watu waliofurika kwenye mitandao ya kijamii wakikejeli Kiingereza cha Shakib kilicho na lahaja nzito ya Kiganda. 

SHAKIB Cham Lutaaya, mfanyibiashara wa Uganda ambaye pia ni mume wa mwanasosholaiti na mjasiriamali Zari Hassan kwa mara ya kwanza amejibu swali la wengi kuhusu alichokifanya kwenye Netflix.


Shakib, ambaye kwa mara ya kwanza katika Maisha yake alitimiza ndoto ya kuonekana kwenye filamu ya Netflix – Young Famous & African, ameelezea kwamba alichokifanya wakati wa kujitambulisha hakikutokea kwa bahati mbaya bali ni jambo ambalo alikuwa akifikiria kwa muda na alifanya hivyo kwa kusudi moja.


Mfanyibiashara huyo ambaye pia ni bondia alifanya mahojiano ya kipekee na kituo kimoja nchini Uganda alipoeleza sababu ya yeye kujitambulisha kwa Kiganda wakati kila mtu alikuwa anatumia lugha ya Kiingereza.


Kwa mujibu wa Shakib, kujitambulisha kwa Kiganda hakukumshusha hadhi kwa njia yoyote kama ambavyo baadhi walihisi kwani alijionea Fahari kuipeleka lugha yake ya nyumbani kwa mamilioni ya watu wanaofuatilia kipindi hicho kote duniani.


Alisema kwamba tangu utotoni, alikuwa akifuatilia filamu na alihisi wakati ajapopata nafasi, ataifanya kwa lugha ya nyumbani kama njia ya kuonyesha fadhila kwa lugha iliyomkuza.


“Nimekua tangu utotoni nikifuatilia filamu za Netflix na nilikuwa nikitamani siku nitaona filamu za Uganda kwenye jukwaa hilo. Hivyo wakati nilipata nafasi ya kuwa kwenye filamu ya Netflix ya Young, Famous & African, nilitaka kupeperusha bendera ya Uganda kwa kutumia lugha ya Luganda,” Shakib alieleza.


Katika filamu hiyo ambayo iliigizwa na matajiri wa fani ya burudani kutoka mataifa kadhaa Afrika, Shakib alijitambulisha kwa lugha ya nyumbani na kuzua maoni kinzani haswa kutoka kwa watu ambao hawana uelewa na lugha hiyo.


Suala hilo bila shaka linadhaniwa kuwa moja ya sababu iliyomfanya mrembo kutoka Nigeria, Anne Macaulay, ambaye hivi majuzi ametalikiwa na mumewe 2Face Idibia kumkejeli Mumewe Zari machoni pa Zari mwenyewe.


Zari pia aliwafunga midomo baadhi ya watu waliofurika kwenye mitandao ya kijamii wakikejeli Kiingereza cha Shakib kilicho na lahaja nzito ya Kiganda.


Kwa mujibu wa Zari, huu umekuwa wakati wa mavuno kwa mumewe na pengine wengi wanaokejeli matamshi yake hawana chochote Zaidi ya simu na ufikiaji wa intaneti.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved