logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Stevo Simple Boy Ajibu Ombi La Irene Nekesa Kumpenda Baada Ya Kuzawadiwa Gari

Hata hivyo, Stevo Simple Boy alionekana kutotongozeka na maneno hayo matamu ya Nekesa akisema kuwa anaelewa vizuri kauli hizo alizozitaja kama ‘mchezo wa taoni’.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani19 February 2025 - 09:21

Muhtasari


  • Katika video hiyo, Nekesa alijimwaya akimwambia Stevo Simple Boy kwamba yeye ndiye anayemfaa, haswa baada ya Stevo kutendwa katika mapenzi kwa mipigo kadhaa.
  • Nekesa aliweka wazi kwamba alikuwa chini ya shinikizo kwa penzi la Stevo Simple Boy haswa baada ya kumuona akiwa na gari hilo jipya.

Stevo Simple Boy amjibu Irene Nekesa kuhusu kumpenda

MSANII Stevo Simple Boy amevunja kimya chake baada ya aliyekuwa mlezi wa wanawe Diana Marua na Bahati, Irene Nekesa kumfungulia moyo kwamba anampenda.

Nekesa katika video moja ambayo ilionekana mitandaoni, alikiri penzi lake kudondokea kwa msanii huyo ambaye sasa ni mmiliki mpya wa gari jijini, aina ya Mazda Demio.

Katika video hiyo, Nekesa alijimwaya akimwambia Stevo Simple Boy kwamba yeye ndiye anayemfaa, haswa baada ya Stevo kutendwa katika mapenzi kwa mipigo kadhaa.

Nekesa aliweka wazi kwamba alikuwa chini ya shinikizo kwa penzi la Stevo Simple Boy haswa baada ya kumuona akiwa na gari hilo jipya.

“Acha niseme ukweli, mimi niko na presha, Stevo Simple Boy amenunua gari na hana bibi. Stevo Simle Boy nakutafuta, uko wapi? Nipigie simu, mimi sitaki kujua gari hilo linaitwa aje, ninachokuambia ni kwamba mimi niko single na wewe pia hauna mtu,” Irene Nekesa alisema.

“Nioe angalau ukilia hapo umepiga magoti nakupangusa machozi. Niko hapa, unataka nikuje nikuoshe miguu, nikupanguse nikufanyiwe masaji, niko hapa kwa ajili yako, uko wapi?” Nekesa aliongeza akisisitiza kwamba moyo wake unadunda kwake Simple Boy.

Hata hivyo, Stevo Simple Boy alionekana kutotongozeka na maneno hayo matamu ya Nekesa akisema kuwa anaelewa vizuri kauli hizo alizozitaja kama ‘mchezo wa taoni’.

“Mchezo wa taoni tunaujua vizuri sana,’ Stevo alijibu huku akiambatanisha jibu lake na emoji za kucheka.

Mapema wiki hii, Stevo Simple Boy alifichua kupokezwa zawadi ya gari jipya aina ya Mazda Demio kutoka kwa muuzaji mmoja wa magari humu nchini.

Akitambulisha zawadi yake jipya kwa mashabiki wake mitandaoni, Stevo Simple Boy alionekana amepiga magoti akisujudu kwa furaha ya kuwa mmiliki wa gari jijini Nairobi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved