logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kijana wa miaka 18 aweka rekodi ya dunia kuwa mtu mwenye nywele nyingi usoni

Lalit Patidar ana hali adimu inayoitwa hypertrichosis, au 'werewolf syndrome' inayosababisha ukuaji wa nywele nyingi usoni.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani13 March 2025 - 10:37

Muhtasari


  • Lalit Patidar ana hali adimu inayoitwa hypertrichosis, au 'werewolf syndrome' inayosababisha ukuaji wa nywele nyingi usoni.
  • Mvulana huyo mwenye umri wa miaka 18, ambaye uso wake umefunikwa na nywele kwa 95%, anasema kuna wale ambao wanaweza kuwa wasio na huruma kwake, lakini ameamua kukumbatia upekee wake.

Lalit Patidar , mshikilizi wa rekodi ya dunia ya Guiness kwa kuwa na nywele nyingi usoni

KIJANA kutoka India amevunja Rekodi ya Dunia ya Guinness kwa sura yenye nywele nyingi zaidi kwa mwanaume.

Lalit Patidar ana hali adimu inayoitwa hypertrichosis, au 'werewolf syndrome' inayosababisha ukuaji wa nywele nyingi usoni.

Mvulana huyo mwenye umri wa miaka 18, ambaye uso wake umefunikwa na nywele kwa 95%, anasema kuna wale ambao wanaweza kuwa wasio na huruma kwake, lakini ameamua kukumbatia upekee wake.

Kwa mujibu wa jarida la Metro UK, Hivi majuzi Lalit alisafiri kutoka nyumbani kwake katikati mwa jimbo la Madhya Pradesh hadi Milan nchini Italia ili kupimwa idadi ya nywele zake kwa kipindi cha TV cha 'Lo Show dei Record'.

Hilo lilihusisha kumtembelea mtaalamu wa trichologist ambaye alinyoa sehemu ndogo za uso wake ili kuchukua vipimo sahihi vya nywele zake kwa kila sentimeta ya mraba, kulingana na Guinness World Records.

Kisha ikafunuliwa alikuwa na nywele 201.72 kwa kila cm ya mraba, na kumfanya rasmi kuwa 'Uso wenye Nywele Zaidi kwa Mtu (Mwanaume)'.

"Lalit ni mojawapo tu ya visa 50 vilivyorekodiwa [vya hypertrichosis] vilivyoripotiwa ulimwenguni kote tangu Enzi za Kati, na kumfanya kuwa mmoja kati ya watu bilioni," Guinness World Records ilisema kwenye tovuti yao.

Kijana huyo alisema ‘hakuwa na neno’ na ‘anafuraha sana’ kutambuliwa kama mshikilizi wa rekodi ya dunia.

Akizungumzia mitazamo ya watu kwake, aliongeza: ‘Watu wengi ni wema kwangu. Inategemea mtu. Siku ya kwanza ya shule haikuwa nzuri sana kwa sababu watoto wengine waliniogopa, lakini waliponijua, walitambua kwamba mimi si tofauti sana nao.’

Baadhi ya watu wamemhimiza kunyoa nywele za usoni, lakini alisema hana mpango wa kufuata ushauri wao.

‘Ninawaambia kwamba napenda jinsi nilivyo na sitaki kubadilisha sura yangu,’ alieleza.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved