logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bifu yangu ya Babu Owino ilianza tukiwania uongozi chuoni Nairobi – Geoffrey Mosiria

Hata hivyo, Babu Owino ambaye anajulikana kuwa kiongozi wa wanafunzi chuoni Nairobi kwa muda mrefu alimshinda Mosiria, uchaguzi ambao Mosiria anadai kwamba ulihitilafiwa kwa faida ya Owino.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani16 March 2025 - 10:48

Muhtasari


  • Kulingana na Waziri huyo wa kaunti, walianza kugombana na Babu Owino wakati wote walijikuta wakiwa washindani wa wadhifa wa rais wa wanafunzi katika chuo cha Nairobi.
  • Hata hivyo, Babu Owino ambaye anajulikana kuwa kiongozi wa wanafunzi chuoni Nairobi kwa muda mrefu alimshinda Mosiria, uchaguzi ambao Mosiria anadai kwamba ulihitilafiwa kwa faida ya Owino.
  • Mosiria alisema kwamba licha ya wote kuondoka katika siasa za chuoni na kujipata katika njia tofauti katika uongozi wa kaunti ya Nairobi, bado anahisi Owino anahisi kuwa yeye ni tishio kwake.

Geoffrey Mosiria

WAZIRI wa mazingira katika kaunti ya Nairobi Geoffrey Mosiria kwa mara ya kwanza amezungumzia kiini cha ugomvi wake na mbunge wa Embakasi Mashariki, Babu Owino.

Akizungumza kwenye runinga ya NTV, Mosiria alifichua kwamba bifu kati yake na Owino haijaanza wakiwa viongozi katika nyadhifa tofauti kwenye kaunti ya Nairobi bali ni ugomvi ambao una mizizi yake tangu wakiwa wanafunzi katika chuo kikuu cha Nairobi.

Kulingana na Waziri huyo wa kaunti, walianza kugombana na Babu Owino wakati wote walijikuta wakiwa washindani wa wadhifa wa rais wa wanafunzi katika chuo cha Nairobi.

Hata hivyo, Babu Owino ambaye anajulikana kuwa kiongozi wa wanafunzi chuoni Nairobi kwa muda mrefu alimshinda Mosiria, uchaguzi ambao Waziri huyo wa kaunti anadai kwamba ulihitilafiwa kwa faida ya Owino.

“Bifu yangu na Babu inarudi nyuma hadi tukiwa chuoni, Babu anaamini kwamba Mosiria hawezi kumshinda. Niliwania dhidi ya Babu Owino katika uchaguzi wa SONU (chuoni Nairobi) na kura ziliibwa kwa faida ya Babu kwa sababu yeye alikuwa ni kibaraka wa uongozi wa chuo. Na bifu hiyo bado ingalipo,” Mosiria alisema.

Mosiria alisema kwamba licha ya wote kuondoka katika siasa za chuoni na kujipata katika njia tofauti katika uongozi wa kaunti ya Nairobi, bado anahisi Owino anahisi kuwa yeye ni tishio kwake.

“Hapa sasa mimi ni afisa mkuu wa mazingira ya kaunti chini ya gavana Sakaja na Babu ni mbunge Embakasi Mashariki. Lakini bado anahisi kwamba mimi ni tishio kwake na pengine anahisi kwamba huenda nitakata kuwania ubunge katika eneobunge lake.”

Afisa huyo wa mazingira hata hivyo alimshauri Owino kutokuwa na wasiwasi anapomuona akifanya mashauriano na vijana katika eneobunge lake wakati amezuru kufanya angalizo kuhusu uchafuzi wa mazingira na kumtaka kuacha kuingilia utendakazi wa kaunti.

“Lakini ningependa kumwambia ndugu yangu, hudumia watu wako kwa heshima na taathima, fany kazi ambapo Mungu amekupa na achene kuingilia utendakazi wetu kama maafisa wa mazingira kwa kuchapisha picha ambapo kuna takataka. Badala yake wewe kama kiongozi toa suluhisho,” Mosiria alimaliza kwa kumshauri Owino.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved