logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Niliteseka naye, sasa ananiacha juu ya slayqueens!” – mke apinga talaka ya mumewe

“Nilisimama naye wakati wa miaka yake ya kuhangaika, nililala njaa na huyu mtu, lakini kwa kuwa ana pesa, anataka kutoroka kuendea slay queens?” Alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani18 March 2025 - 10:19

Muhtasari


  • “Nilisimama naye wakati wa miaka yake ya kuhangaika, nililala njaa na huyu mtu, lakini kwa kuwa ana pesa, anataka kutoroka kuendea slay queens?” Alisema.
  • Lakini Norman katika utetezi wake, alidai kuwa mkewe amekuwa akicheza na hirizi na alihofia maisha yake.

Mahakama

DRAMA ilijiri katika mahakama moja baada ya mwanamke kupinga vikali uamuzi wa mumewe kutaka kumtaliki akisema kwamba hawezi kubali talaka hiyo kwa kile anahisi si uamuzi sahihi wa mumewe.

Mwanamke huyo aliyetambulika kwa jina Noreen, alipinga vikali kwamba hawezi kubali talaka kutoka kwa mumewe Norman, kwani walitafuta mali wote na sasa mume anataka kumuacha kwa kuendea vidosho wabichi.

Norman, ambaye aliingia mahakamani kwa kujiamini akitarajia talaka ya haraka, alikabiliwa na upinzani mkali.

Noreen, ambaye amekuwa kando yake kwa karibu miaka 30, alikataa kutia sahihi hati za talaka, akisema kwamba hakuvumilia miaka mingi ya kuteseka naye ili mwanamke mwingine aje kufurahia maisha ya mafanikio na mumewe.

"Kwa nini nimuache kwa kuwa amefanikiwa, wakati nilisimama naye wakati wa miaka yake ya kuhangaika, nililala njaa na huyu mtu, lakini kwa kuwa ana pesa, anataka kutoroka kuendea slay queens?” Alisema.

Lakini Norman katika utetezi wake, alidai kuwa mkewe amekuwa akicheza na hirizi na alihofia maisha yake.

"Mheshimiwa, nilimshika mkono mkali akijaribu kuniroga, sitaki kuamka hata siku moja akageuka chura!" alilamika na kupeleka chumba cha mahakama katika kicheko.

Kulingana na Noreen, matatizo halisi yalianza 2018 binti yao alipougua. Alitaja kuwa baadhi ya ndugu walishuku uchawi, lakini badala ya kusikiliza, Norman alichukua kama uthibitisho kuwa yeye ni mganga aliyeidhinishwa.

Tangu wakati huo, mambo yalikuwa yamepungua, huku akiwa nje ya nyumba kila mara, akinong'ona kwenye simu yake kama msichana.

"Mtu huyu hayupo nyumbani, huwa anatuma meseji kwa wasichana wadogo, basi siku moja tunasikia kwamba amempa mtu mwingine mimba?" Alisema, akipiga makofi kwa kuchanganyikiwa.

Wawili hao waliofunga ndoa mwaka wa 1995 baada ya Norman kulipa mahari na wana watoto sita pamoja.

Sasa, mume anasisitiza kwamba anataka kutoka, lakini Noreen anasema haendi popote.

 

 

 

Hakimu akitamani angekuwa na kinywaji baridi kupunguza joto la ukumbi wa mahakama, aliahirisha kesi hiyo kwa ajili ya hukumu.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved