logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ Shiti aeleza kwa nini anahisi msanii chipukizi Nexxie atasumbua sana sanaa ya Kenya

Ungamo la Shiti kuhusu ubora wa chipukizi huyo linajiri wakati Zuwena anasuta Wakenya, akisema kuwa wangekuwa wanajua kumshika Nexxie mkono, angekuwa miongoni mwa majina makubwa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani25 March 2025 - 14:40

Muhtasari


  • Shiti alisema kuwa msanii huyo ana sauti nzuri, utunzi mzuri na wa kipekee ambao unaleta ladha halisi ya Kikenya kwenye masikio ya wapenzi wa muziki.
  • “Anaitwa Nexxie Music msanii chipukizi kabisa kutoka +254, huyu anaenda kusumbua sana sanaa ya muziki. Talanta tupu kutoka Kenya. Nexxie hii nimeweka tiki,” Dj Shiti alisema 

DJ Shiti ampigia upato msanii chipukizi, Nexxie Music//FACEBOOK

SIKU chache baada ya Zuwena Platnumz kudai kwamba atamkwapua msanii chipukizi wa Kenya, Nexxie na kumpeleka Tanzania ili kumkuza kimuziki, mchekeshaji wa humu nchini, Dj Shiti naye amekariri kwamba kipaji cha msanii huyo ni kikubwa ajabu.

Katika video ambayo inaenezwa mitandaoni, DJ Shiti alirekodi video akifurahia moja ya ngoma za Nexxie Music na kutabiri kwamba chipukizi huyo akiendelea kwa kasi hiyo, huenda akawavuruga sana wasanii wakubwa Kenya.

Kwa mujibu wa Shiti, Nexxie Music ana fursa nzuri ya kujikweza na kuwa uso mpya wa muziki wa Kenya, haswa baada ya wengi wa wasanii tegemezi kuonekana kulegeza kamba na kupunguza kasi katika kuachia miziki ya kuwakosha mashabiki wa Kenya.

Shiti alisema kuwa msanii huyo ana sauti nzuri, utunzi mzuri na wa kipekee ambao unaleta ladha halisi ya Kikenya kwenye masikio ya wapenzi wa muziki.

“Anaitwa Nexxie Music msanii chipukizi kabisa kutoka +254, huyu anaenda kusumbua sana sanaa ya muziki. Talanta tupu kutoka Kenya. Nexxie hii nimeweka tiki,” Dj Shiti alisema katika video hiyo.

Ungamo la Shiti kuhusu ubora wa chipukizi huyo linajiri wakati ambapo mrembo aliyepata umaarufu baada ya kucheza kama pambo kwenye video ya Zuwena ya Diamond Platnumz kuwasuta Wakenya, akisema kuwa wangekuwa wanajua kuwashika machipukizi wao mikono, basi Nexxie angekuwa miongoni mwa majina makubwa.

Mrembo huyo alitishia kumchukua Tanzania na kumsimamia kimuziki huku akiwatahadharisha Wakenya dhidi ya kukurupuka kuwa ni wao wakati nyota yake itakapong’aa.

“Wakenya wanapenda kuongea sana lakini kupigana support hawawezi. Kitu kidogo wanapakini, mbona mnapaniki Kenya, mbona? Wakenya mnajua kuongea sana lakini hamwezi ku’support wenzenu,” alitupa jiwe kwa Wakenya.

 “Mimi nataka nimchukue huyu Nexxie nimlete Tanzania nimsimamie kimuziki ila akijak ufikia kiwango Fulani wasije kudai kwamba ooh ni msanii wetu wakijibvunia. Hawawezi jivunia kwa sababu mimi nitakuwa nimembadilisha kuwa wa huku,” aliongeza. 

Nexxie Music ni moja kati ya majina ya ajabu yaliyoteka maskio ya wapenzi wa muziki nchini Kenya tangi mwaka jana.

Msanii huyo kwa sasa anatamba na kibao chake cha ‘We Hafi Do It’ ambacho kilitoka takribani wiki mbili zilizopita.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved