logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Wakenya mnaongea sana lakini hamjui ku’support wasanii wenu” – Zuwena Platnumz

Zuwena alisema kwamba ana mpango wa kumchukua msanii chipukizi – Nexxie Music - kutoka Kenya na kumpeleka kwao Tanzania kumsimamia katika masuala ya kimuziki kwa lengo la kumuinua.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani20 March 2025 - 09:57

Muhtasari


  • “Wakenya wanapenda kuongea sana lakini kupigana support hawawezi. Kitu kidogo wanapakini, mbona mnapaniki Kenya, mbona?"
  • "Wakenya mnajua kuongea sana lakini hamwezi ku’support wenzenu,” alitupa jiwe kwa Wakenya.

Zuwena Platnumz

RECHO Elias, maarufu kama Zuwena wa Diamond amewatupia dongo kubwa Wakenya kwa kile anahisi kwamba wana tantarira nyingi sana lakini vitendo sifuri.


Akizungumza kwenye klipu moja, vixen huyo aliyepata umaarufu miaka miwili iliyopita baada ya kutumika kama mpambe kwenye video ya wimbo wa Diamond Platnumz ‘Zuwena’ alisema kwamba ana mpango wa kumchukua msanii chipukizi kutoka Kenya na kumpeleka kwao Tanzania kumsimamia katika masuala ya kimuziki kwa lengo la kumuinua.


“Wakenya wanapenda kuongea sana lakini kupigana support hawawezi. Kitu kidogo wanapakini, mbona mnapaniki Kenya, mbona? Wakenya mnajua kuongea sana lakini hamwezi ku’support wenzenu,” alitupa jiwe kwa Wakenya.


Zuwena alisema kwamba japo wengi wanahisi Bien ndiye msanii bora kutoka Kenya – haswa baada ya kushinda tuzo ya Trace kama msanii bora wa ukanda wa Afrika Mashariki akiwapika wengine kama Diamond, kwake yeye msanii chipukizi kwa jina Nexxie ndiye msanii bora.


“Sisi Tanzania [kimuziki] ni wakali sana, lakini Kenya wana mtu wao mmoja tu ambaye mimi namkubali. Ni nanajua tena anajua sana. Ni msanii mmoja hivi ambaye anaitwa Nexxie, msanii mkali sana,” Zuwena alisema.


Zuwena alisema kwamba Nexxi Music, japo ni chipukizi lakini anajua sana sit u kuimba, bali pia kuandikwa nyimbo na hata kwenye kutumbuiza mubashara.


“Kwanza anajua kuimba, hata kwenye performance anajua kucheza na steji. Ila sasa wao Wakenya hawawezi waka support msanii wao wa Kenya. Wanachojua ni maneno mengi.”


Akitangaza mpango wa kumchukua na kumsimamia kimuziki, Zuwena alitoa onyo kwa wakenya wasije wakaanza kudai kwamba Nexxi ni wao baada yake yeye kumpaisha ngazi kumuziki.


 “Mimi nataka nimchukue huyu Nexxie nimlete Tanzania nimsimamie kimuziki ila akijak ufikia kiwango Fulani wasije kudai kwamba ooh ni msanii wetu wakijibvunia. Hawawezi jivunia kwa sababu mimi nitakuwa nimembadilisha kuwa wa huku,” aliongeza. 

Nexxie Music ni moja kati ya majina ya ajabu yaliyoteka maskio ya wapenzi wa muziki nchini Kenya tangi mwaka jana.


Msanii huyo kwa sasa anatamba na kibao chake cha ‘We Hafi Do It’ ambacho kilitoka takribani wiki mbili zilizopita.


Msanii huyo amefanya ngoma kadhaa ikiwemo kolabo na mkali wa Dancehall, Redan – kibao kwa jina Vile Inafaa lakini pia ana ngoma zake mwenyewe kama Far, Hela, We Gide More, Shake Up miongoni mwa nyingine.


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved