logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Diamond ana ubinafsi ndio maana anahisi eti naweza mrudia wakati wowote!” - Zari

Zari alisema kwamba kwa upande wake haoni kama Diamond ana kile kinachohitajika ili kumrudisha kwake, kinyume na jinsi Diamond alidai kwamba Zari anatamani kumrudia.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani16 March 2025 - 11:34

Muhtasari


  • Akizungumza pindi alipotua nchini Kenya, Zari aliitaja kauli hiyo ya babydaddy wake kama ubinafsi wa hali ya juu, akionekana kuikanusha.
  • Zari alisema kwamba kwa upande wake haoni kama Diamond ana kile kinachohitajika ili kumrudisha kwake, kinyume na jinsi Diamond alidai kwamba Zari anatamani kumrudia.

Diamond na babymama wake Zari Hassan

SOSHOLAITI na mfanyibiashara wa Uganda mwenye makao yake Afrika Kusini, Zari Hassan amezungumzia kauli aliyoitoa Diamond Platnumz kwenye kipindi cha uhalisia cha Netflix kwamba mama huyo wa Watoto 5 anaweza mrudia wakati wowote.

Akizungumza pindi alipotua nchini Kenya, Zari aliitaja kauli hiyo ya babydaddy wake kama ubinafsi wa hali ya juu, akionekana kuikanusha.

Zari alisema kwamba kwa upande wake haoni kama Diamond ana kile kinachohitajika ili kumrudisha kwake, kinyume na jinsi Diamond alidai kwamba Zari anatamani kumrudia.

"Diamond anasema chochote anachojisikia kwa sababu inalisha ubinafsi wake. Diamond ana ubinafsi, na unahitaji kulishwa kila wakati. Lakini sio juu ya kile anachosema - je, ninafanya hivyo? Je, ni kweli kwamba anaweza kumrudisha tena Zari?” Zari alisema.

Hata hivyo, Zari alisema kwamba yeye hana tatizo na Diamond kwani mwisho wa siku anasalia kuwa baba kwa wanawe wawili na hawezi badilisha uhalisia huo.

Mjasiriamali huyo alisema kwamba kwa kipindi ambacho amemjua Diamond, anamuelewa kwamba ni mtu mwenye majivuno na ubinafsi mwingi, hivyo akimsikia akitoa kauli ya kujigamba, yeye anajua fika kwamba huo ni ubinafsi wake unazungumza na hawezi kuchukia.

"Kwa hivyo kwangu, mimi ni kama, nah, hiyo ni ego yako tu, na niko sawa na hilo."

Kauli yake inajiri wiki kadhaa baada ya Diamond katika sehemu yake kwenye kipindi cha Young Famous and African kwenye Netflix alisema kwamba yeye ako na kila kinachohitajika kumrudisha Zari kwake.

Katika mahojiano hayo, Diamond alikariri kwamba Zari hawezi kataa ombi la kurudi kwake ikiwa angelipendekezewa, akiashiria kwamba Zari bado ana hisia za mapenzi kwake.

Hii ni licha ya kila mmoja kusonga mbele na maisha yake, Diamond sasa akiwa katika uhusiano na msanii wa lebo yake, Zuchu huku Zari akifunga ndoa ya Nikkah na mpenzi wake Shakib Cham Lutaaya.

Kulingana naye, ziara yake nchini Kenya inahusiana kabisa na biashara, na ana miradi kadhaa iliyopangwa.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved