logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zari akiri kumwambia Fantana kwamba Diamond ana mpenzi mwingine Tanzania

Baada ya mahusiano kati ya Diamond na Zari kuvunjika, Zari aliolewa na Shakib Lutaaya ambaye ni mwanabiashara nchini Uganda.

image
na Japheth Nyongesa

Mastaa wako12 March 2025 - 12:34

Muhtasari


  • Zari kwenye mahojiano na mwanahabari amesema kwamba ni ukweli na hata watu wa Tanzania wanafahamu hilo.
  • Mwanadada huyo alifichua hayo na kueleza kwamba siyo yeye peke aliyemwambia Fantana hata wasani wengine wa kike walimufichulia.

caption
ZariHasan maarufu 'Zari the boss lady' ambaye ni mzaliwa wa Uganda amekiri kwamba ni yeye aliyemchochea Diamond kwa Fantana na kumueleza kwamba mwanamuziki huyo wa Wasafi ana mpenzi mwingine Tanzania.

Zari kwenye mahojiano na mwanahabari amesema kwamba ni ukweli na hata watu wa Tanzania wanafahamu hilo. Mwanadada huyo alifichua hayo na kueleza kwamba siyo yeye peke aliyemwambia Fantana hata wasani wengine wa kike walimufichulia.

"Nilimwambia kwani ni uwongo, mpaka kina Nadia wamemwambia kitu hicho hicho, Kanye amemwambia, kuna dada mwingine hapo Rozeti amemwambia kweli Diamond ana mtu kule," alifichua Zari.

Mwanamziku huyo tokea Uganda amesisitiza kwamba kumwambia Fantana kuhusu mahusiano ya Diamond si wivu maana kwa sasa hata yeye ana mtu wake.

"Nyinyi ni wa Tanzania kwani nilisema uwongo? ..Yaani acha nikwambia kabisa hainihusu sasa hivi. Mimi kukuambia hivyo haimaanishi chochote, sai mimi naangalia kuwa mwanamke tofauti wa baadaye. Sasa mimi imeonekana ni kama nina wivu, mimi namwambia sina shida 'Diamond' yuko na mtu wake na mimi nina mtu wangu," alisema Zari.

Mwanamziki Zari na nyota wa bongo fleva Tanzania Diamond Platinumz waliwahi kuwa kwenye mahusiano ya mapenzi kwa muda mrefu. Wawili hao wana watoto wawili ambao wamezaa pamoja.

Baada ya mahusiano kati ya Diamond na Zari kuvunjika, Zari aliolewa na Shakib Lutaaya ambaye ni mwanabiashara nchini Uganda.

Zari na Fantana hawaonani macho kwa macho. Mwanadada Zari aliwahi kukiri kwamba hana chuki juu ya Fantana na Diamond kuwa kwenye mahusiano ila aliudhika na vitendo vyao vya kumuongelelea hadharani.

Sikuwa na wivu na yule binti, shida yangu ni kwa baba ya mtoto wangu Diamond, amekaa na mwanamke mwingine akinijadili, namheshimu Diamond sana, yeye ni baba wa watoto wangu na siku zote tutakuwa na uhusiano huu, lakini ukikaa na kunijadili na kumpa mtu mwingine ujasiri wa kuninyanyasa hapo ndipo unapovuka mpaka, "Zari alisema.

"Siwezi kukaa na mume wangu sasa hivi na kuanza kumjadili Diamond, kamwe. Diamond angeweza tu kumtongoza msichana huyu bila kutumia jina langu na najua inawezekana,' alisema Zari awali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved