logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond aonyesha dalili za kumsajili msanii mwingine kwa lebo ya Wasafi baada ya Mbosso kuondoka

Msanii Nasibu Abdul Juma Issack alimaarufu Diamond ameashiria dalili za kumsajili msanii mpya Katika lebo ya WASAFI

image
na Evans Omoto

Mastaa wako19 March 2025 - 12:16

Muhtasari


  • Msanii huyo wa Tanzania alitangaza mkataba wa makubaliano kati ya kampuni yake na mwimbaji mpya akiashiria kipaji kingine kipya  chaja aliandika katika ukurasa wake wa Instagramu.
  • Wasafi Limited (WCB) kampuni iliyosajiliwa kwa sheria za Tanzania kufanya shuguli za sanaa yenye makao yake Mbezi Beach, S.L.P 105260, Dar es Salaam (katika mkataba huu itajulikan kama hivi karibuni kwa kumtaja msanii huyo’’ aliendelea kutoa maelezo.

Msanii Nasibu Abdul Juma Issack alimaarufu Diamond ameashiria dalili za kumsajili msanii mpya Katika lebo ya WASAFI baada ya Mbosso kuondoka.

Msanii huyo wa Tanzania alitangaza mkataba wa makubaliano kati ya kampuni yake na mwimbaji mpya akiashiria kipaji kingine kipya  chaja aliandika katika ukurasa wake wa Instagramu  pasi kumtaja jina msanii huyo.

‘’Mkataba wa kujiunga na kampuni ya muziki. Mkataba huu unaingiwa leo terehe 18 mwezi 03, 2025,”Diamond alisema.

Hio ilikuwa ishara tosha kuwa  Diamond alikuwa  mbioni kumsakama na kumpata nyota mwingine wa muziki ambaye atazidi kutamba  na kutaratamba katika Nyanja na katika sanaa hiyo ya kimziki.

Kwa kuzungumzia kuondoka kwake Msanii Mbosso Diamond aliweza kusema kuwa urafiki wao na Mbosso ulikuwa wa viwango vikubwa hata kufikia uamuzi wa kuondoka kwake.

‘’Mbosso wiki mbili na nusu nyuma tumeongea na Mbosso na aliniomba aweze kujisimamia na nikampa baraka zangu zote."

Mbosso ni mdogo wangu nikamwambia Mbosso tumeishi vizuri na hatujawai gombana na wala hatujawai kwazana na kwa jinsi ulivyo niheshimu kwa kunipenda na tukapendana siwezi kukutoza hata shilingi na sijamtoza hata shilingi kumi,” Diamond alifafanua katika mahojianao na kituo kimoja cha habari.

Msanii Diamond alizidi kumsifia na kumwita Mbosso kama rafiki yake tena wa dhati katika masuala mbalimbali  ya Kisanaa na kwa kushirikiana jambo ambalo lilisababisha kutomtoza hata senti moja alipotaka kuondoka.

‘’Kwanza ninamshukuru kwa kutumia hekima. Unajua ni wasani wachachwe wanaweza kutumia hekima hiyo kwa sababu kwanza alivyokuja Mbosso alikuwa amekuja kulipa lakini nikwamwambia, bro, tumeishi vizuri nawe na kwa heshima uliyonipa siwezi nikakutoza chochote. Namna nilivyoishi na Mbosso, kumtoza hela ni aibu kwangu. Angekuwepo mtu mwingine ambaye hatujaheshimiana hela unatoa,” alisema.

Hata hivyo kinachosubiriwa kwa sasa na washabiki wa Diamond ni kumuona msanii huyo ambaye wana uchu na ari kuu ya kumuona na kumuweka kwenye mizani ya Wasafi iwapo ataafikia viwango vyake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved