logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Dimitri Payet: Mchezaji wa zamani achunguzwa kumtesa mpenziwe kunywa mkojo wake

"Aliniomba uthibitisho wa mapenzi, ambao ulikuwa na udhalilishaji. Nilirekodi video nikinywa mkojo wangu, kunywa maji kutoka kwenye bakuli la choo.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani15 April 2025 - 11:14

Muhtasari


  • "Mnamo Desemba, tuligombana kwa mara ya kwanza na akaanza kuniambia kuwa angeniadhibu," alisema.
  • "Aliniomba uthibitisho wa mapenzi, ambao ulikuwa na udhalilishaji. Nilirekodi video nikinywa mkojo wangu, kunywa maji kutoka kwenye bakuli la choo na kulamba sakafu," alisema.

Dimitri Payet

MWANAMKE raia wa Brazil anayedai kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanasoka wa Ufaransa Dimitri Payet amewasilisha malalamiko dhidi yake mjini Rio de Janeiro kwa "unyanyasaji wa kimwili na kisaikolojia", kulingana na ripoti ya AFP.

Katika kesi hiyo iliyoangaziwa na France24, mrembo huyo anayedai kuwa mpenzi wa zamani wa Payet alimnyanyasa kiasi kwamba alilazimika kunywa mkojo wake mwenyewe ili kudhihirisha mapenzi yake kwake.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 38, ambaye alitumia muda mwingi wa uchezaji wake na Marseille kila upande wa Ligi Kuu akiwa na West Ham United, alijiunga na Vasco da Gama mnamo 2023, na kuwasili Rio na mkewe na watoto.

Kulingana na ripoti ya polisi, ya Machi 29, mwanamke huyo alisema "alishambuliwa" na Payet, na kumwachia alama kwenye mwili wake, na kudhulumiwa "kimwili, kimaadili, kisaikolojia na kingono", France24 waliandika.

Mlalamikaji, wakili mwenye umri wa miaka 28 na mfuasi wa Vasco da Gama, aliiambia AFP kwamba alikutana na Dimitri Payet kupitia Instagram Agosti mwaka jana, na kwamba walikuwa na uhusiano wa kimapenzi.

"Mnamo Desemba, tuligombana kwa mara ya kwanza na akaanza kuniambia kuwa angeniadhibu," alisema.

"Aliniomba uthibitisho wa mapenzi, ambao ulikuwa na udhalilishaji. Nilirekodi video nikinywa mkojo wangu, kunywa maji kutoka kwenye bakuli la choo na kulamba sakafu," alisema.

Mwanamke huyo pia alidai kuwa wakati mwingine Payet "alimsukuma" na "kumkanyaga".

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved