logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana aamrisha polisi kuwakamata watu wenye dreadlocks na kuwanyoa kwa lazima!

"Hakuna mtu anayepaswa kubeba aina yoyote ya nywele ndani ya Minna. Nimetoa amri za kuandamana kwa vyombo vya usalama," alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani23 April 2025 - 11:22

Muhtasari


  • "Hatutavumilia ukatili wowote. Mtu yeyote utakayemkuta ana dreadlocks, mkamate, nyoa nywele na mtoze faini.”
  • "Hakuna mtu anayepaswa kubeba aina yoyote ya nywele ndani ya Minna. Nimetoa amri za kuandamana kwa vyombo vya usalama," alisema.

Vijana wenye nywele za Rasta//HISANI

HUKU visa vya uhalifu na mashambulizi ya majangili yakiendelea kuripotiwa katika Maeneo mbalimbali nchini Nigeria, gavana wa jimbo la Niger, Umar Bago ametoa amri ya kukamatwa na kunyolewa kwa mtu yeyote mwenye rasta.

Katika video iliyosambazwa mitandaoni ambapo alikuwa Akizungumza katika mkutano wa usalama wa wadau uliofanyika katika Ikulu ya Serikali Jumanne, gavana huyo alisema nywele za watu hao zinafaa kukatwa na kutozwa faini.

"Hatutavumilia ukatili wowote. Mtu yeyote utakayemkuta ana dreadlocks, mkamate, nyoa nywele na mtoze faini.”

"Hakuna mtu anayepaswa kubeba aina yoyote ya nywele ndani ya Minna. Nimetoa amri za kuandamana kwa vyombo vya usalama," alisema.

Kwa mujibu wa jarida la PUNCH, Mkutano huo ulihudhuriwa na vyombo vya usalama na watawala wa kimila.

Aliwataka wazazi kuwaonya watoto wao, akisema serikali itaanza kutekeleza hatua kali za usalama.

"Wazazi wanapaswa kuwaonya watoto wao. Kuanzia wakati huu, ni 100% ya kulipa moto kwa moto.”

"Pia, nyumba yoyote itakayopatikana ikiwa na wahalifu inapaswa kubomolewa. Jimbo la Niger si la watu wasio na manufaa," gavana Bago aliongeza.

Pia alitangaza vizuizi vya usafirishaji wa pikipiki za kibiashara na tuktuk kati ya saa kumi na mbili jioni na saa kumi na mbili asubuhi huko Minna, akibainisha kuwa ni zile tu zinazotumika kwa dharura za matibabu ndizo zitaruhusiwa kuhudumu kwa muda wote.

Gavana wa jimbo la Niger, Umar Bago//FACEB0OK

Aidha mkuu huyo wa jimbo aliwaagiza viongozi wa mitaa, wakiwemo wakuu wa wilaya, vijiji na kata, kuhakikisha wanaweka kumbukumbu sahihi za wakazi katika jamii zao.

Aliongeza kuwa mali yoyote itakayotumika kuwahifadhi wahalifu au kuuza dawa za kulevya itaharibiwa.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved