logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mafisi poleni!Kutana na mpenzi wake msanii Nadia Mukami

Kulingana na msanii huyo Mpenzi wake ambaye alimtambulisha kama Priyan amekuwa naye kwa njia zake

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 May 2021 - 14:25

Muhtasari


  • Msanii Nadia Mukami ni mmoja wa wasanii ambao wametia bidii katika tasnia ya burudani licha ya kuwa na changamoto tofauti
  • Hongera sana Nadia, kamati ya mafisi poleni ashaanyakuliwa na mwingine
nadia-mukami-341

Msanii Nadia Mukami ni mmoja wa wasanii ambao wametia bidii katika tasnia ya burudani licha ya kuwa na changamoto tofauti.

Wengi wamekuwa wakiuliza msanii huyo kama anampenzi lakini leo kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amewashangaza mashabiki wake baada ya kupakia picha ya mpenzi wake huku akimsifia.

Kulingana na msanii huyo Mpenzi wake ambaye alimtambulisha kama Priyan amekuwa naye kwa njia zake panda na katika changamoto zake.

"Licha ya kila kitu walichosema juu yangu leo, umenioga kwa upendo mimi natabasamu tu hapa karibu na wewe

Kuwa katika umaarufu, unahitaji mtu anayekupenda, Mtu anayekuona nje ya umaarufu, pesa, umakini, uvumi, mazungumzo na matusi

Mtu ambaye anazungumza na nafsi yako na wewe ni hivyo tu! Nilipaswa kukutana nawe mapema ili nipate aina hii ya mapenzi lakini najua haijachelewa

Tunatoka makabila 2 tofauti lakini Upendo wetu unashinda hilo! NAKUPENDA SANA PRIYAN💕,"Aliandika Nadia.

Hongera sana Nadia, kamati ya mafisi poleni ashaanyakuliwa na mwingine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved