logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ninampeza, lakini ilibidi nimuache aende,'Zari asema baada ya kufuta picha akiwa na mpenzi wake

Katika ujumbe wake wa siri, Zari alisisitiza kwamba ilimbidi amwache aende

image
na Radio Jambo

Habari05 July 2021 - 10:24

Muhtasari


  • Zari afuta picha akiwa na mpenzi wake mitandaoni

Mfanyabiashara wa Uganda anayeishi Afrika Kusini Zari Hassan ameibua wasiwasi kati ya wafuasi wake milioni 9.3 baada ya kuweka ujumbe wa siri, ambao sasa umehusishwa na uhusiano wake mpya.

Zari amefuta picha zote alizowahi kupiga na mpenzi wake anayejulikana kama Dark Stallion, kitu ambacho kimewaacha mashabiki wengi wakiwa na wasiwasi.

Katika ujumbe wake wa siri, Zari alisisitiza kwamba ilimbidi amwache aende kwa sababu hawakusaidiana  kwa njia yoyote.

“Ninampeza, lakini ilibidi nimuache aende. Ikiwa haijengi mimi sitaitunza," Aliandika Zari.

Zari alifunua uso wa mpenzi wake mpya mnamo Februari 14, baada ya miezi ya kumuweka mbali na macho ya umma.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza, wanamitandao kumuona "Dark Stallion" kwani picha zote za awali alipigwa akiwa ameficha uso wake.

Kufunuliwa kulikuja siku ’baada ya kushambuliwa  na wakosoaji ambao walikuwa wakidai kuwa mapenzi na " Dark Stallion "hayatadumu.

Sosholaiti huyo alisema kuwa hajali ikiwa uhusiano huo utadumu au la, lakini alikuwa tayari na wakati mzuri na mpenzi wake mpya.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved