logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Amber Ray asherehekea siku ya kuzaliwa ya Jimal Rohosafi huku Amira akiipuuza

Amira ameonekana kupendelea kuchapisha matangazo ya kibiashara badala ya kumpakia mfanyibiashara huyo ambaye alitishia kutaliki takriban mwezi mmoja uliopita.

image
na Radio Jambo

Michezo31 December 2021 - 11:03

Muhtasari


•Amira ameonekana kupendelea kuchapisha matangazo ya kibiashara badala ya kumpakia mfanyibiashara huyo ambaye alitishia kutaliki takriban mwezi mmoja uliopita.

Amber Ray, Jimal Rohosafi, Amira

Mwenyekiti wa muungano wa wahudumu wa matatu  jijini Nairobi Jamal Marlow Rohosafi anasherehekea siku yake ya kuzaliwa hivi leo. (Desemba 31)

Mamia ya wanamitandao wamejitokeza kusherehekea pamoja na mfanyibiashara huyo hukuwakimwandikia  jumbe nzuri za kheri ya kuzaliwa.

Mwanasoshalaiti mashuhuri Faith Makau almaarufu kama Amber Ray hajaachwa nyuma katika kumsherehekea baba huyo wa watoto wawili na ambaye anaaminika kuwa mpenzi wake.

"Kheri za siku ya kuzaliwa mwenyekiti.. cheers kwa nyingi zaidi" Amber Ray amemwandikia Jimal.

Mke wa Jimal, Amira hata hivyo ameonekana kupuuzilia siku hiyo maalum maishani mwa baba ya watoto wake wawili.

Kwenye ukurasa wake wa Instagram, Amira ameonekana kupendelea kuchapisha matangazo ya kibiashara badala ya kumpakia mfanyibiashara huyo ambaye alitishia kutaliki takriban mwezi mmoja uliopita.

Mnamo mwezi Novemba Amira alielekea mahakamani akiomba kutenganishwa na Jimal baada yake kumsherehekea Amber Ray alipokuwa anaadhimisha siku yake ya kuzaliwa.

Inaaminika kwamba Jimal na Amber Ray wamerudiana baada ya kutengana mapema mwaka huu. Siku za hivi majuzi wawili hao wamekuwa wakionekana pamoja mara nyingi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved