logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera!Milly Wajesus na Kabi Wajesus watarajia mtoto wao wa pili

Siku ya JUmanne wawili hao waliwatangazia mashabiki wao kwamba wanatarajia mtoto wao wa pili.

image
na Radio Jambo

Habari18 January 2022 - 15:03

Muhtasari


  • Milly Wajesus na Kabi Wajesus watarajia mtoto wao wa pili

Wanabiashara na wauanda maudhui Milly Wajesus na Kabi Wajesus, wamepata wafuasi wengi mitandaoni kutokana na video zao wanazopakia kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii na kwenye mtandao wa Youtube.

Licha ya changammoto abazo wawili hao wamekuwa wakikumbana nazo kwenye ndoa yao, wamewahakikishia mashabiki wao kwamba ndoa ni kitu muhimu maishan.

Siku ya JUmanne wawili hao waliwatangazia mashabiki wao kwamba wanatarajia mtoto wao wa pili.

Kupitia kwenye ukurasa wa Milly wa Instagram alimshukuru MUngu kwa kumpa nafasi nyingine ya kuwa mzazi.

"Tunayo furaha kubwa hatimaye kushiriki habari za kusisimua na familia yetu mtandaoni. FAMILIA YA WAJESUS INAENDELEA NA TUNAMPA MUNGU UTUKUFU WOTE. Ametuchagua kuwa wazazi kwa mara nyingine tena na kuunganisha pamoja mdogo ili kujiunga na familia yetu.

Kwa @kabiwajesus sikuwahi kufikiria njia bora zaidi ya kushiriki baraka zetu na familia yetu ya mtandaoni,"Milly na Kabi Waliandika.

Tunawatakia kila la Kheri katika safari yao.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved