logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Niko single!" Amira athibitisha kutengana na mfanyibiashara Jimal Rohosafi

Mama huyo wa watoto wawili amesisitiza kuwa kwa sasa hategemei jasho la mwanamume yeyote na kile anachopata kinatokana na bidii yake.

image
na Radio Jambo

Habari20 January 2022 - 08:02

Muhtasari


•Mama huyo wa watoto wawili amesisitiza kuwa kwa sasa hategemei jasho la mwanamume yeyote na kile anachopata kinatokana na bidii yake.

Amira na aliyekuwa mumewe Jimal Rohosafi

Mjasiriamali Amira na ambaye alikuwa mke wa mwenyekiti wa Muungano wa Wamiliki wa Matatu jijini Nairobi Jimal Marlow Rohosafi amethibitisha kwamba ndoa yao iligonga mwamba.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Amira ameweka wazi kwamba kwa sasa hana mchumba na  anajitegemea mwenyewe.

Mama huyo wa watoto wawili amesisitiza kuwa kwa sasa hategemei jasho la mwanamume yeyote na kile anachopata kinatokana na bidii yake.

"Siku nyingine tu ya kukukumbusha kuwa sina mchumba na ninatia bidii kubwa kupata mali yangu mwenyewe" Amira amesema.

Haya yanajiri takriban miezi miwili baada ya malkia huyo kudai talaka kutoka kwa aliyekuwa mume wake Jimal Rohosafi.

Amira alionekana kukerwa na uhusiano kati ya mume wake na mwanasoshalaiti Amber Ray na kudai kuwa hangeweza kuvumilia katika ndoa hiyo.

Ni hatua ambayo nilifaa kupiga kitambo lakini sikuwa na ujasiri. Lakini inafika wakati  ambapo unasema imetosha! Leo nimefika mwisho, natumai hatua hii itawapatia wengine ujasiri wa kuacha yale ambayo yanawavuta nyuma. Nafanya juhudi kuwa bora na kuangalia watoto wangu, na kufanya biashara yangu. Hatua moja kwa wakati" Amira alisema mnamo mwezi Novemba.

Baadaye Amira alionekana katika mahakama ya Kadhi ambako aliwasilisha ombi la kumtaliki mfanyibiashara huyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved