logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Siwezi kuwa mpweke siku hii ya wapendanao,'Mwanamume atangaza kumpenda Betty Kyallo

Betty alijibu akisema atamtafuta Skytone baadaye ili wakanywe kahawa.

image
na Radio Jambo

Habari14 February 2022 - 11:50

Muhtasari


  • Betty yallo amjibu mwanamume aliyetangaza kumpenda

Mwanamume Mkenya aliyetambulika kwa jina la Skytone Baby anatafuta uchumba na Betty Kyallo,Skytone anasema ameamua kukiri haya  kwani Betty ndiye mwanamke anayefanya mapigo yake ya moyo kuongezeka.

Akiingia mitaani, Skytone aliandika bango akisema hataki kusherehekea siku ya wapendanao peke yake.

“Mimi ni Skytone baby, siwezi kuwa mpweke siku ya Valentine,Ninamtafuta mpenzi wangu, mrembo Betty Kyallo. Wana Nairobi wananiunganisha,” aliandika Skytone kabla ya kusambaza nambari yake.

Betty alijibu akisema atamtafuta Skytone baadaye ili wakanywe kahawa.

"Heri ya wapendanao wote. Pia kwa Muungwana huyu, asante kwa upendo. Acha nikununulie kahawa wakati mwingine."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved