logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je, Harmonize anamkosa Kajala? Vipi kuonekana kwenye bango?

Harmonize - Kila mtu katika Konde Gang anajua kwamba nakukosa sana

image
na Radio Jambo

Habari28 March 2022 - 08:15

Muhtasari


• "Unaweza niona na niamini mimi, sina furaha. Kila mtu katika Konde Gang anajua kwamba nakukosa sana" - Harmonize 

Harmonize

Baada ya uvumi kusambaa mitandaoni kwamba msanii Harmonize bado analikosa sana penzi na uwepo wa muigizaji mkongwe wa filamu za bongo, mwanamama Fridah Kajala, hatimaye msanii huyo amelitema dukuduku lake la moyoni.

Wikendi iliyopita, aliachia ujumbe tata kwenye instastories zake ambapo aliweka wazi kwamba anamkosa sana Kajala katika maisha yake licha ya kuwa katika penzi lingine na mwanadada mzungu.

“Unaweza niona na niamini mimi, sina furaha. Kila mtu katika Konde Gang anajua kwamba nakukosa sana,” aliandika harmonize.

Japo hakumtaja mlengwa wa ujumbe wenyewe, lakini wengi walihisi kwamba huu ujumbe kwa njia yoyote ile utakuwa umeelekezwa kwa Kajala.

Hii si mara ya kwanza kwa msanii huyo kubainisha na kudhihirisha wazi mapenzi yake kwa mwanamama Kajala ambaye kwa wakati mmoja walikuwa katika mapenzi kabla ya Sakata la Harmonize kumtaka kimapenzi mwanawe Kajala, Paula ambaye ni mpenzi wa Rayvanny.

Tetesi hizi kuhusu kumkosa Kajala zinakuja muda mchache tu baada ya bango kubwa kuonekana Harmonize akiwa na Kajala ambapo limeambatanishwa na neno “Lovers”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved