logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Daddy tuonyeshe njia" Akothee amsihi Ezekiel Mutua kutajirisha wanamuziki wa Kenya

Amemwomba Mutua kuwasaidia wasanii kuweza kuvuna mazao ya kazi zao.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 April 2022 - 08:19

Muhtasari


•Akothee amemwomba Mkurugenzi Mtendaji huyo wa zamani wa KFCB kuwasaidia wasanii kuweza kuvuna mazao ya kazi zao.

•Mutua alisema lengo lake ni kuona wanamuziki wa Kenya wametajirika, wameheshimika na kupata ushawishi mkubwa. 

Mwanamuziki Esther Akoth almaarufu kama Akothee ameikaribisha ahadi ya bosi mpya wa MCSK, Ezekiel Mutua kuwa atawakwamua wanamuziki wa Kenya kutoka  kwenye ufukara.

Akothee amemwomba Mkurugenzi Mtendaji huyo wa zamani wa KFCB kuwasaidia wasanii kuweza kuvuna mazao ya kazi zao.

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 42 alikuwa anaunga mkono kauli ya Mutua kuwa "Inauma sana kuona wanamuziki wakiandaa harambee wanapougua."

"Daddy tuonyeshe njia, tumechoka kuonewa," Akothee alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Katika taarifa yake ya hivi majuzi, Mutua alisema lengo lake ni kuona wanamuziki wa Kenya wametajirika, wameheshimika na kupata ushawishi mkubwa. 

Alisema haridhishwi na hali ya sasa ya wanamuziki wa Kenya huku akiahidi kutia juhudi kuhakikisha kwamba wamesaidika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved