logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hatimaye Carol Sonnie avunja kimya kufutia madai ya kushangaza ya Mulamwah dhidi yake

Mulamwah alishangaza wengi baada ya kudai kwamba yeye sio baba mzazi wa binti wa Muthoni.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 April 2022 - 08:53

Muhtasari


•Muthoni amezamia kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuchapisha ujumbe ambao umeoneka kuzungumzia yale yanayoendelea.

•Hapo awali Muthoni alipotembelea studio zetu alisisitiza kwamba yupo tayari kufanya DNA iwapo itabidi.

Carrol Sonnie katika studio za Radio Jambo

Hatimaye mwigizaji Caroline Muthoni amezungumza baada ya aliyekuwa mpenzi wake David Oyando almaarufu Mulamwah kuibua kapu la madai ya kushangaza kumhusu.

Hivi majuzi Mulamwah alimshtumu Muthoni kwa kutokuwa mwaminifu wakati wa mahusiano yao, kupachikwa ujauzito na jamaa mwingine kati ya madai mengine mengi.

Muthoni amezamia kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuchapisha ujumbe ambao umeoneka kuzungumzia yale yanayoendelea.

"Maisha yanapokupa sababu mia za kuangua kwa kilio, onyesha maisha kuwa una sababu milioni za kutabasamu na kushukuru. Kuwa na nguvu," Muthoni aliandika.

Mulamwah alishangaza wengi siku ya Ijumaa baada ya kudai kwamba yeye sio baba mzazi wa binti wa Muthoni. 

Wanamitandao wameendelea kutoa hisia tofauti kuhusiana na madai hayo, baadhi wakimshtumu huku wengine wakipendekeza vipimo vya DNA vifanyike.

Hapo awali Muthoni alipotembelea studio zetu alisisitiza kwamba yupo tayari kufanya DNA iwapo itabidi.

Kwa kipindi cha takriban miezi sita ambacho kimepita Mulamwah amekuwa akisisitiza kwamba  mtoto huyo ni wake hadi Ijumaa alipobadilisha msimamo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved