logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Harmonize kumfikia Diamond, aah bado sana!" - Baba Levo

Baba Levo - Harmonize Hana Uwezo wa kutengeneza Kiki ya Kumfunika Diamond Platnumz, Kwa Vyovyote Vile.

image
na Radio Jambo

Habari22 April 2022 - 07:55

Muhtasari


• Baba Levo - “Nishasema Mtu yeyote atakaejaribu Kushindana na Diamond Ataishia Vitu Vingi,”

Harmonize, Baba Levo, Diamond Platnumz

Msanii na mtaalamu wa ujenzi Baba Levo amemchamba Harmonize kwa mara nyingine tena na kusema kwamba mkurugenzi huyo wa Konde Music Worldwide hana uwezo hata chembe kumzima Diamond Platnumz kwa lolote iwe kimuziki au hata kufanya kiki.

Kulingana na Baba levo, Harmonize bado hajai hata kwenye kiganja cha Diamond kwani ni kama mtoto tu anayejaribu kuiga babake wa muziki lakini ameshindwa na kuamua kutumia njia hasi ya kutembeza chuki na matusi dhidi yake mitandaoni badala ya kujitahidi kumfikia na akishindwa kumfikia basi arudi kujiunga naye kumshabikia.

“Harmonize Hana Uwezo wa kutengeneza Kiki ya Kumfunika Diamond Platnumz, Kwa Vyovyote Vile Hana Uwezo wa Kuzima EP ya FOA,” Baba Levo alisema.

Chawa huyo wa Wasafi pia alizidi kutilia mkazo kwamba amesema mara nyingi tu kwamba si Harmonize pekee bali msanii yeyote atakayedanganyika kuchukua mkondo wa kujaribu kushindana na Diamond basi atapoteza vingi, yaani itakuwa kama ng’ombe anayejaribu kushindana na ndovu kunya, bila shaka atakwama kwenye gogo la tembo.

“Nishasema Mtu yeyote atakaejaribu Kushindana na Diamond Ataishia Vitu Vingi,” alisisitiza kutoa onyo hilo Baba Levo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved