logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kiasi cha pesa alichoibiwa Jalang'o na waliokuwa wafanyikazi wake

Hii ni baada ya waliokuwa wafanyakazi wake kuiba pesa, kutoka kwa gari walilokuwa wanaosha na kutoroka.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri07 June 2022 - 12:45

Muhtasari


  • Hii ni baada ya waliokuwa wafanyakazi wake kuiba pesa, kutoka kwa gari walilokuwa wanaosha na kutoroka
Jalango

Wikendi iliyopita haikuwa ya furaha kwa mwaniaji ubunge wa Lang'ata, mcheshi na mtangazaji Jalang'o.

Hii ni baada ya waliokuwa wafanyakazi wake kuiba pesa, kutoka kwa gari walilokuwa wanaosha na kutoroka.

Habari hizo zilitangazwa na Jalang'o,ilhali hakufichua kiasi cha pesa walichoiba, huku akitoa zawadi kwa mtu yeyote atakaye onyesha walipokuwa wafanyakazi hao.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram Jalang'o alisema kuwa;

"Eli na Litiema wako mbioni, leo asubuhi waliiba pesa kwenye gari walilokuwa wakiosha nyumbani, simu zao hazipo na wanakimbia na familia zao. Ukiwaona tafadhali wasiliana 0722915337 au toa taarifa katika kituo cha polisi kilicho karibu nawe Zawadi ya 100k kwa taarifa yoyote itakayopelekea kukamatwa kwao."

Rafikiye  Jalang'o, Billy Miya alidai kuwa wafanyikazi hao wawili walitoroka na KSh 2.5 milioni.

"Weuh! Shetani ni mtu mubaya sana.Unahustle na boss wako for more than 4 years, ile mwaka anaenda kuingia bunge shetani anakudanganya unaiba 2.5M.Yaani si mungesubiri boss aingie Bunge mukuwe mafutani.Jamani tupige ripoti polisi Au piga 0722 717 159.Pole sana Jalango Mwenyewe itakua sawa.Uzuri alitupeleka moja kwa moja hadi kwao kupitia social media.Over to you DCI Kenya,"Billy alifichua.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved