logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sitawahi msahau ex wangu Wolper-Juma Jux akiri

Jux alisema, "Wote wawili ni warembo, kila mmoja ana plus/faida zake kwa njia tofauti."

image
na Radio Jambo

Habari13 June 2022 - 11:43

Muhtasari


  • Huku akiwa kwenye mahojiano na Wasafi, akijibu swali ni ex yupi bora zaidi maishani mwake kati ya Jackline Wolper na Jackie Cliffe alisma kwamba hatawahi msahau Wolper
Juma Jux

Hata baada ya kuvuma sana mitandaoni wiki chache zilizopita baada ya madai ana uhusiano na mwanasosholaiti Huddah Monroe Juma Jux amekiri hatawahi msahau mmoja wa ex wake.

Huku akiwa kwenye mahojiano na Wasafi, akijibu swali ni ex yupi bora zaidi maishani mwake kati ya Jackline Wolper na Jackie Cliffe alisma kwamba hatawahi msahau Wolper.

"Eh, nani alikuwa bora zaidi wa zamani? Unataka nifanye wapi hii? Ni lazima nichague? Dah! Hii ni ngumu wanaume, Hii ​​ni hivyo. ngumu kwa sababu kila hatua ninapitia kwenye maisha yangu kila moja ni muhimu, Ila kama ningechagua ningesema ni Wolper. I will never forget my ex-Wolper."

Akijibu picha ya Huddah Monroe na aliyekuwa mpenzi wake Vanessa Mdee, almaarufu Vee Money kwenye skrini, Jux aliulizwa aeleze anapendelea nani.

"Kusema kweli wote ni warembo na wa ajabu kwa namna yao. Wasichana wote ni pisi ni wazuri hapa. Vanessa ni mrembo, Huddah, ni mrembo pia. Unataka nichague nani mzuri zaidi?"

Jux alisema, "Wote wawili ni warembo, kila mmoja ana plus/faida zake kwa njia tofauti."

Lil Ommy hakushawishika na kumtaka Jux azikadirie kwa asilimia.

Jux alisema, "Waah, wote wana plus yao, kuna vitu wamezidiana. Kuna vitu navipenda kila mmoja wao kivyake, kitu ninavyo penda kwa Huddah, kuna vitu ninavyopenda kwa Vee."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved